Sarah Kaisi aka Shaa anahisi kolabo nyingi za kimataifa ni za
kulazimisha, hugharimu fedha nyingi na wala hazina manufaa kwa wasanii
wengi wa Kibongo.
Akiongea na safu ya Starehe ya gazeti la Mwanancho, Shaa amesema hana mpango wa kufanya kolabo za aina hiyo.
“Siwezi kufanya kolabo na staa yeyote wa kimataifa,” alisema. Mimi
nipo kibiashara zaidi na ni ngumu kwangu kwa sababu nahitaji kufanya
muziki nipate fedha. Hizi kolabo za kimataifa unajikuta ukimlipa pesa
mhusika huku wewe ukiingia gharama ya kusafiri huko na kurekodi. Kama
unavyojua, inachukua muda na gharama kubwa, nahitaji kufanya kitu
ambacho nitafaidika nacho na siyo kunipotezea fedha.”
“Asilimia kubwa kolabo hizo ni za kulazimisha na kupoteza pesa, siyo
za kuuza au kumwingizia kipato mhusika. Unatakiwa ufanye kolabo, kisha
upate shoo kubwa za kurudisha gharama uliyotumia. Lakini nionavyo mimi
nyingi ni za kutafuta ujiko tu, siwezi kufanya kolabo na D Banj kisha
isiniingizie chochote.”
Credits: Mwananchi
Post a Comment