
Watu
wasiojulikana wamevunja ghala la kuhifadhia dawa zilizokwisha muda wake
wa matumizi katika hospitali ya wilaya ya Makete mkoani Njombe na kuiba
dawa zilizokwisha muda wake wa matumizi na kutokomea nazo
kusikojulikana
Tukio
hilo la aina yake limetokea usiku wa kuamkia jana januari 21, 2014 na
kuzua sintofahamu na hali ya taharuki kwa wakazi wa Makete mkoani Njombe
baada ya kusikia taarifa hiyo
Akizungumzia
tukio hilo Mganga mfawidhi hospitali ya wilaya ya Makete Dkt. Michael
Gulaka amesema tayari wameshatoa taarifa kwenye kituo cha polisi
wilayani hapo na kuwataka wananchi kuwa makini wanapokwenda kununua dawa
kwenye maduka ama kwa watu kuangalia tarehe ya matumizi ya dawa hiyo
ili kuepuka kuuziwa dawa zilizokwisha muda wake wa matumizi
Dkt.
Gulaka amesema kwa mujibu wa taratibu za kiafya, dawa hizo zilizoibiwa
ni sumu kwa kuwa muda wake wa matumizi umekwisha na hivyo zilikuwa
zikisubiri kwenda kuteketezwa lakini kabla ya zoezi hilo kufanyika ndipo
wizi huo umetokea
Ametoa
rai kwa wananchi kutoa taarifa polisi ama hospitali ya wilaya ya Makete
pindi watakapoona dawa zikiwa zimezagaa mitaani ama kuwa na mashaka na
dawa watakazoziona mahali popote na kuzitilia shaka ili watuhumiwa hao
wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria
إرسال تعليق