Msanii wa muziki aliyefanya vizuri kipindi cha nyumba MB Dog
amesema msanii bila kuwa na management ni sawa na kufanya kazi bila
malengo.
Ameiambia Bongo5 kuwa amehangaika kufanya muziki peke yake bila mafanikio ndio maana aliamua kurejea Tip Top Connection.
“Tip Top nilitoka na ndio kitu ambacho kilinirudisha nyuma sana,”
amesema. “Pale nilikuwa nafanyiwa kila kitu, nilikuwa narekodi tu kazi
yangu vitu vingine vyote wanafanya wao so baada ya kutoka na kujisimamia
mwenyewe nikaanza kuyumba na kuhangaika huku na kule. Kwahiyo kitu
ambacho nimegundua msanii bila management nzuri huwezi fika mbali
asikwambie mtu. Msanii anahitaji kuongozwa, kushauriwa na mambo mengine.
Sasa hivi nipo Tip Top tumeingia makubaliano mapya ya kazi ndio maana
nashukuru Mungu ngoma yetu mpya ‘Umenuna’ inasonga kidogo kidogo mpaka
kieleweke.”
Post a Comment