TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 28.03.2014




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 28.03.2014

Mnamo tarehe 28.03.2014 majira ya saa 02:10 usiku huko Gulwe katika Wilaya ya Mpwapwa kulitokea ajali ya treni ya mizigo iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kwenda Kigoma baada ya kusombwa na mkondo wa maji ya mvua zinazoendelea kunyesha. Kutokana na wingi na nguvu ya maji hayo ilifanya kichwa cha treni hiyo kutumbukia kwenye mto Mimo.


VIFO:
Ajali hiyo hadi hivi sasa imesababisha vifo vya watu wawili ambao wamefahamika kwa majina yafuatayo:-
1.  Felix s/o Kalonga
2.  Ismail @ Suma

MAJERUHI:
Waliojeruhiwa ni kama ifuatavyo:-
1. Hassan s/o Kitambo, Mhehe, Miaka 89, Mkazi wa Kidete – Amelazwa katika Hospitali ya Mpwapwa.

2. Reuben Ngasongwa, Miaka 43 – Amehamishwa kutoka Hospitali ya Wilaya Mpwapwa kupelekwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro.

3.Michael Lupatu, Mbondei, Miaka 52 – Amehamishwa kutoka Hospitali ya Mpwapwa kwenda Hospitali ya Mkoa wa Morogoro.

4.  Ramadhan Kanenda, Miaka 34, Mnyamwezi – Amelazwa Mpwapwa Hospitali.
5.Mohamed Salum, Miaka 25,  - Alitibiwa na kuruhusiwa
6. E.2699 CPL Mfaume – Ametibiwa na kuruhusiwa.
7.E.3295 CPL Respis – Bado amelazwa Mpwapwa Hospitali.

Bado jitihada za kuwatafuta watu wengine wanne ambao hawajulikani walipo zinaendela.

Imetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma

Post a Comment

أحدث أقدم