

Umati wa watu waliohudhuria 
maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar 
yanayoendelea hivi sasa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, 
maonyesho haya yanajumuisha shughuli mbalimbali zikiwemo maonyesho. 
Maadhimisho haya yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoaka mataifa 
mbalimbali
 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la Jeshi la wananchi kwenye sherehe za miaka 50 ya Muungano wa Tanzania.
 Kikosi cha Makomandoo kikipita kwa mwendo wa aina yake wakati wa sherehe za miaka 50 ya Muungano.
 Sehemu ya wageni
 waalikwa waliohudhuria sherehe za miaka 50 ya Muungano ambazo 
zimefanyika katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
 Kikosi cha 
Makomandoo kikitoa salaam kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
katika sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Muungano.
 Makomandoo wakionyesha namna ya kupambana bila kutumia nyenzo hapa wakivunja matofali kwa kutumia kichwa na mikono.
 Baadhi ya silaha zakijeshi zikipitishwa mbele ya umati kuonyesha uwezo mkubwa wa jeshi letu.
 Kikosi cha Wanamaji 
 Ndege za kivita 
zikilinda Ndege ya Rais katika maonyesho ya Ndege yaliofanyika kwenye 
Kilele cha  Maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano.
 Askari wa kikosi cha Mwamvuli akishuka kutoka futi 4500 kwenye uwanja wa Uhuru kwenye kilele cha miaka 50.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpa mkono wa pongezi mmoja wa wanajeshi wa kikosi cha mwamvuli .
 Maandamano ya Pikipiki.
 Matembezi maalum ya kusheherekea miaka 50 ya Muungano .
Njiwa wakirushwa juu kama ishara ya miaka 50 ya Muungano ambapo watu waliorusha njiwa hao nao wametimiza miaka 50.














Post a Comment