Rais Omar al Bashir wa Sudan amesema baadhi ya madola makubwa duniani yanataka Sudan mbili ziungane tena.
Akihutubia
wajumbe wa chama tawala cha Kongresi ya Taifa ya Sudan, Al Bashir
amesema madola kadhaa duniani yameomba radhi kwa sababu ya kuunga mkono
kutengana kwa Sudan mbili.
Rais wa
Sudan amebainisha kuwa baada ya Sudan Kusini kujitenga na Sudan, maadui
wa Khartoum walishangazwa na muqawama ulioonyeshwa na Sudan baada ya
utengano huo, na leo hii wanaonyesha kujuta na kuitaka Sudan ikubali
suala la kuungana tena Sudan mbili.
Amesema
kuungana sehemu nyengine na ardhi ya Sudan, mbali na kuhitajia ridhaa ya
serikali kutalazimu pia kuitishiwa kura ya maoni ili kupata msimamo wa
wananchi.
Itakumbukwa
kuwa asilimia 99 ya wakaazi wa Sudan Kusini waliunga mkono kujitenga
eneo hilo na Sudan katika kura ya maoni iliyoitishwa mwezi Januari mwaka
2011, na mnamo tarehe 9 Julai mwaka huo huo Sudan Kusini ikajitangazia
uhuru na kujitenga rasmi na Sudan.
Baadhi ya
duru za habari zimefichua kuwa viongozi wa Marekani na Umoja wa Ulaya
wanahisi kwamba katika hali iliyopo hivi sasa ni muhali kwa nchi mbili
za Sudan na Sudan Kusini kuishi kwa amani na masikilizano na hivyo
wanazitaka nchi hizo zikubali kuanzisha shirikisho la mkataba mkabala na
kupatiwa msaada mkubwa wa fedha na madola makubwa duniani.
Source: kiswahili.irib.ir

إرسال تعليق