Chidi Benz na Mchezo wa kupiga watu - Makala

20140424-213139.jpg


MWANAISHA – “Chidi naona uko na mama watoto”
CHIDI BENZ – “kusogea karibu nikakuta ni Mwanaisha na wenzake, ndio nikamwambia mbona unanichora au kwasababu nipo na dem mkali kuliko wewe?…..unaona wivu?…. kilichofata ni chupa ambayo Mwanaisha aliirusha ikanipata kichwani na kunipasua damu zikatoka ndipo mimi nikamshika
nywele Mwanaisha na baada ya hapo kilichofata sikumbuki maana nilikua nimelewa” (Kwa Mujibu wa DJFetty blog)
Hii ni sababu ambayo Chidi Benz msanii mkubwa tu hapa nchini ameitoa kupitia “Gossip Cop Soody Brown” wa segment cha “You Heard” ndani ya XXL ya Clouds FM baada ya mtangazaji huyo kwenda kumtembelea kituo cha polisi cha sehemu hiyo mitaa ya ILALA magorofani.
Kweli kwa msanii ambae anaongoza kwa mskendo za kupiga watu ambao hawajawahi kusema, watangazaji wa maradio, wasanii wenzake na kuwasababishia majeraha makubwa kwa kipindi kirefu anaweza akatoa sababu kama hiyo ambayo imefikia kumsababishia maumivu makali mwanadada “Mwanaisha” ambae hata kama kweli alimuita na kumwambia maneno hayo yeye kama kioo cha jamii alitakiwa kufanya matendo hayo kweli?…. Chidi Benz ni msanii mzuri sana mwenye kipaji lakini hivi sasa mashabiki wake wameacha kusikiliza muziki wake na kukaa kusikiliza skendo ambazo ni uchafu wa tabia isiyokubalika katika jamii ya karne hii, huwezi kuamka na kuanza kumshambulia binadamu mwenzako haswa mwanamke na kuweza kumsababishia majeraha ya kuweza kushonwa nyuzi 18.
Haya ni matendo ambayo Jamii haitakiwi kukubaliana nayo kwa watu kama hawa, vyombo vya habari visibaki kukimbizana na kuwasaidia kupromote nyimbo zao na kuwachekea na umaarufu wao wakati huku kwenye jamii wanafanya mambo yasiyostahili kuwepo kwa watu wa aina hiyo sababu wanaishia mtaani kuhatarisha usalama wa wananchi haswa haswa wanawake ambao ndio wanaoonewa sana na watu hawa. Juzi tumetoka kusikia DUDU BAYA amemkata sikio “Mama yake amkubwa” ambae ni mwanamke mwenye umri mkubwa kutokuwa na nguvu za kuhimili na kuzuia shambulio la mtu “Mwanaume” mwenye mwili mkubwa kama DUDU BAYA huko Mwanza na leo tunakuja kusikia Chidi Benz amefanya kitendo hicho hicho kwa mwanamke hapa Dar Es Salaam.
Hata kama ni wasanii na wanajulikana na kujuana na Police, lakini haki lazima itendeke tena kwa mfano dhahili kama wao ni vioo vya jamii ili wananchi wa kawaida wasije wakafwata matendo hayo yasiyo mazuri. Matendo hayo tumeona hata nchini Marekani msanii “Chris Brown” baada ya kumshambulia “Rihanna” pamoja na umaarufu wake wote, hivi sasa anatumikia kifungo Jela baada ya kutoka Rihab kwa makosa yake aliyoyatenda.
Chidi Benz ambae kutokana na vyombo vya habari kuwa anashikiliwa na polisi baada ya kesi kwenda mahakamani ambapo Mheshimiwa “Hakimu” ameamuru kuendelea kushikiliwa kwa kwa msanii huyo baada ya hali ya Mwanaisha kuwa mbaya kiasi cha kushindwa kuongea.
20140424-213110.jpg

Post a Comment

Previous Post Next Post