MrJazsohanisharma

Justin Bieber afanya “Suprise” kwa watoto YATIMA, akiwa nchini JAPAN.

bl64rpuiyaa-nht


Justin Bieber ni mmoja wa wasanii wachache kabisa wanaofatiliwa sana na vyombo vya habari dubiani kwa sasa, Siku za karibun Justin amenaswa na vyombo mbalimbali vya habari akifanya matendo ambayo yamewaacha watu midomo wazi. Machache kati ya hayo ni kukamatwa na madawa na ya kulevya, kelewa kupitiliza na kuendesha gari kwa kasi huku akijua kabisa leseni yake imeisha mda wa matumizi. Matendo haya yalifikia kufikishwa Ikulu ya nchini Mareaki “White House” na baadhi ya wananchi wa nchi hiyo kutaka afutiwe ‘Hati’ yake ya kuishi nchini humo ili arudi kwao nchini Canada.
Justin ambaye kwa sasa yupo nchini Japan huku akiwa kasindikizwa na mama yake mzazi ‘Patti Mallette’ na watu wa karibu wa Justin Bieber. Akiwa nchini humo Justin aliamua kutembelea kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo nchini humo, Kupitia akaunti yake ya Instagram Justin aliweka video ikimwonyesha akicheza na watoto hao.
Tukio la Justin Bieber kutembelea kituo hicho limechukuliwa tofauti huku wengine wakimpongeza kwa kutembelea kituo hicho huku wengine wakisema kua Justin kaamua kufanya hivyo ili kuwalaghai watu ili wasahau mabaya yake.

Post a Comment

أحدث أقدم