Mkurugenzi
wa Masoko Airtel Tanzania Levi Nyakundi akiongea na waandishi wa habari
wakati wa kufunga kliniki ya kimataifa ya soka ya siku tano ya Airtel
Rising Stars kwenye uwanja wa Azam Compex. Kliniki hiyo ilileta pamoja
vijana zaidi ya 70 kutoka nchi 12 Barani Afrika.
Kocha
Neil Scott kutoka shule za soka ya vijana za Manchester United akiongea
kwenye sherehe za kufunga kliniki ya soka ya kimataifa ya Airtel Rising
Stars kwenye uwanja wa Azam Compex. Kliniki hiyo ilileta pamoja vijana
zaidi ya 70 kutoka nchi 12 Barani Afrika. Pamoja naye ni Andrew Stoke
kutoka MUSS and Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Levi Nyakundi.
.Washiriki watajuwa kuwa na malengo ya kujiunga na timu zao za taifa pamoja na klabu zinazoshiriki ligi kuu.
.Mwisho wa kliniki ni mwanzo wa msimu wa wa Airtel Rising Stars kwa nchi 17.
Kliniki
ya siku tano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars imefikia tamati jana
huku washiriki wakiwa na shauku kubwa ya kutumia ujuzi waliopata kwa
kuwa nyota wa soka kwenye nchi zao na hata wa kimataifa.
Kliniki
hio iliodhuriwa na washiriki zaidi ya 70 kutoka nchi za Kenya, Malawi,
Sierra Leone, Burkina Fasso, Chad, Congo Brazzaville, DRC, Niger,
Madagascar, Gabon, Shelisheli na wenyeji Tanzania. Makocha kutoka shule
za soka ya vijana wa Manchester United ndio walioendesha kliniki hiyo.
Kliniki
hiyo imetoa fursa kwa washiriki kuendelea kukuza vipaji vyao chini ya
programu ya shule za soka ya vijana za Manchester United, ambazo ni
maarufu kwa kufundisha jinsi ya kucheza kandanda safi na la kushambulia.
Makocha hao wawili – Neil Scott na Andrew Stokes walikuwa wakitoa
mafunzo kwa kuengemea upande wa ufundi, ujuzi na nidhamu ndani na nje ya
uwanja.
‘Makocha
kutoka Manchester United kwa kushirikiana na Airtel wamefanya kazi kubwa
kuwafundisha hawa vijana na naomba shirikisho la Mpira katika kila nchi
pamoja na vilabu vya ligi kuu kuwapa nafasi kuendeleza vipaji vyao,’
alisema Levi Nyakundi, Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania wakati wa
kufunga kliniki hiyo kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Aliongeza,
‘Airtel inatambua baadhi ya vijana wa Airtel Rising Stars wamekuwa
wakishiriki kwenye timu za vijana tangu kuanzishwa kwa programu hii. Ni
matarajio yetu kwamba washiriki wengi wa Airtel Rising Stars watapata
nafasi ya kucheza kwenye timu za miaka chini 20. Tumepata nguvu ya
kuendelea kuwekeza kwenye programu hii kwa sababu tumeweza kuona
mafanikio yake.’
Airtel
Rising Stars ni mpango kambambe kwa Afrika kuwapa fursa kwa wasichana na
wavulana wenye umri chini ya miaka 17 kuonyesha vipaji vyao kwa waalimu
waliobobea kwenye masuala ya kandanda na kupata nafasi ya
kuziendeleza.
Kocha
Mkuu wa timu ya Taifa ya wanawake Rogasiana Kaijage ambaye amefuatilia
mafunzo hayo tangu mwanzo hadi mwisho amesisitiza umuhimu wa klabu
kuwekeza kwenye vijana wenye umri wa chini kulikon kutumia fedha nyingi
kununua wachezaji ambao umri ushakwenda. Kaijage amesema programu kama
hizi zinasaidia kupata vipaji chipukizi lakani kazi ya kuviendeleza
inabakia kuwa ya klabu.
Kumalizika
kwa kliniki nii kutoa nafasi nyingine kwa Airtel Rising Stars kuzindua
awamu ya nne ya programu hii ambayo uanzia kwenye ngazi ya kata mpaka
Taifa kwa nchi kumi 17 Barani Afrika, ambapo Airtel inafanya biashara.
Mchezaji
wa timu ya Sierra Leone ya Airtel Rising Stars Fatmata Mansaroly,
akipokea cheti kutoka kwa Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Levi
Nyakundi baada ya kumalizika kwa kliniki ya soka ya kimataifa ya Airtel
Rising Stars kwenye uwanja wa Azam Compex. Kliniki hiyo ilileta pamoja
vijana zaidi ya 70 kutoka nchi 12 Barani Afrika. Kushoto ni Meneja
Uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando
Mchezaji
wa timu ya Tanzania ya Airtel Rising Stars Joseph Prosper, akipokea
cheti kutoka kwa Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Levi Nyakundi
baada ya kumalizika kwa kliniki ya soka ya kimataifa ya Airtel Rising
Stars kwenye uwanja wa Azam Compex. Kliniki hiyo ilileta pamoja vijana
zaidi ya 70 kutoka nchi 12 Barani Afrika. Kushoto ni Meneja Uhusiano
Airtel Tanzania Jackson Mmbando.
Timu
ya Tanzania ya Airtel Rising Stars wakiwa kwenye picha ya pamoja baada
ya kumalizika kwa kliniki ya siku tano ya soka ya kimataifa ya Airtel
Rising Stars kwenye uwanja wa Azam Complex. Waliokaa kutoka kushoto ni –
Kocha mkuu wa timu ya Wanawake Tanzania Rogasian Kaijage, Mkurugenzi
Masoko Airtel Tanzania Levi Nyakundi na Makocha kutoka shule za soka ya
vijana za Manchesterb United Neil Scott na Andrew Stokes.
Post a Comment