Madee aungana na mama yake kusherehekea siku ya kuzaliwa na watoto yatima Kibaha Maili Moja

1MADEE
Msanii wa muziki Madee leo anaungana na mama yake kwenda kusherehekea siku yake ya kuzaliwa na watoto yatima wa kituo cha Hope kilichopo Kibaha Maili Moja, Mkoa wa Pwani.
Madee amesema kuwa ameamua kufanya hivyo kama sehemu ya kuirudishia jamii na kumshukuru Mungu.
“Naelekea Kibaha kwenda kukaa na mama yangu na familia yangu pia. Kwa ujumla kuna kituo pale kinaitwa Hope cha watoto yatima,nitatoa kile ambacho nimekipata mwaka mzima. Kwahiyo naona ni muhimu kushukuru kwasababu ninaweza nisifike mwakani. Lazima kushare na watu wengi furaha yako.Baadaye baadae tutatoa taarifa tunakutana wapi. Lakini najaribu kuongea na Marco Chali ambaye ni rais wa Mbudya, aniunganishe kule. Namshukuru Mungu, wadau wote wa muziki pamoja na mashabiki wangu kwa kunifikisha hapa.”

Post a Comment

Previous Post Next Post