News:- Jay Z anusurika kupigwa $100,000 kwa mzigo wake wa Thamani ya $20 Million.

20140423-003635.jpg
collection ya nyimbo za Jay Z ambazo ni “master recordings” ambazo zilipotea mnamo mwaka 2002 zimepatikana mjini Califonia kwenye Storage Unit zilipokuwa zimechimbiwa na producer Chauncey Mahan, producer huyu ambae aliwahi kufanya kazi na Jay Z kuanzia miaka ya 1998-2002, alibanwa na polisi siku ya ijumaa kuhusiana na mzigo huo baada ya kukamatwa nao ambao unasadikika kuwa na thamani ya $15 – $20 Million lakini hakufunguliwa mashtaka. TMZ wameripoti.
Mahad aliwasiliana na ‘Live Nation’ ambao ni joint venture na kampuni ya msanii huyo ‘Rock-A-Fella Records’ alisema atapiga mnada mzigo huo au alipwe kiasi cha dola za kimarekani laki moja ($100,000) kwa ajili ya kuhifadhi mzigo kwa muda wote huo. Walikubaliana kumalizana kwa $75,000 na kukubaliana kukutana mitaa ya North-ridge California, kwa malipo hayo na ili kuweza kukabidhiana mizigo hiyo bila kujua kuwa kampuni hiyo ya Jay Z walikuwa wameshawasiliana na Polisi ambao walimtia hatiani na kuzuia mzigo huo mpaka siku ya Mahakama ambapo Judge atakapoamua nani akabidhiwe mali hiyo.

Post a Comment

أحدث أقدم