Benki ya NMB imezindua rasmi tawi lake jipya mjini Kigoma.
Uzinduzi wa tawi hilo lililoko katika jengo la Bima barabara ya Lumumba
katika jengo la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ulifanyika mwishoni mwa
wiki. Aidha, tawi hilo lililo mkabala na Soko Kuu la Kigoma, limelenga
kutoa huduma kwa watu binafsi na wakazi wengi wa maeneo hayo hususan
wafanya biashara ndogo ndogo.
![DSC_0935](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/04/DSC_0935.jpg)
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kigoma
Bw.Ramadhani Maneno alisema tawi hilo litasaidia kusogeza karibu huduma
za kifedha kwa wakazi wa Kigoma kutokana na mkoa huo sasa kupata
maendeleo ya kiuchumu na kijamii.“Binafsi naishukuru NMB kwa juhudi zake
za kuboresha huduma zake kwa lengo la kukidhi matakwa ya wateja na
kuwafikia katika maeneo mbalimbali chini,” alisema Maneno.
![DSC_0967](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/04/DSC_0967.jpg)
Kwa upande wake, Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi, Bw. Abraham
Augustine alisema,”Tumekuwa tukifanya jitihada za kuhakikishia kwamba
benki hii inatoa huduma bora kwa wateja wetu wengi. Katika juhudi hizi,
tumekuwa tukipanua mtandao wa matawi kuhakikisha kwamba tupo katika
maeneo jirani na wateja wetu.”
![DSC_0969](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/04/DSC_0969.jpg)
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Bw. Charles Gichilu (kulia) akipata huduma kutoka benki ya NMB. Pembeni yake ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bw. Ramadhani Maneno
![DSC_0891](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/04/DSC_0891.jpg)
Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo
![DSC_0969](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/04/DSC_0969.jpg)
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Bw. Charles Gichilu (kulia) akipata huduma kutoka benki ya NMB. Pembeni yake ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bw. Ramadhani Maneno
![DSC_0891](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/04/DSC_0891.jpg)
Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo
إرسال تعليق