Papa Francis awatangaza Mapapa John XXIII na John Paul II watakatifu(Picha)

article-0-1D64727100000578-57_964x642
Waumini wa kanisa katoliki wakifuatilia sherehe za kutangazwa watakatifu mapapa John XXIII na John Paul II
 Mapapa wa zamani, John XXIII na John Paul II wametangazwa watakatifu Jumapili hii na Papa Francis hafla iliyoshuhudiwa na umati mkubwa wa waumini wa kanisa katoliki kwenye viwanja vya St. Peter’s Square, jijini Vatican.

Mamilioni ya watu wengine duniani wameangalia kupitia runinga tukio hilo la viongozi wa zamani wa kanisa katoliki wakipewa utakatifu.
Vatican ilitarajia watu milioni 1 kukusanyika kwenye kanisa hilo pamoja na barabara za kuelekea kwenye kanisa la St. Peter’s Basilica. Sherehe hizo zimehudhuriwa na makadinali 150, maaskofu 1,000 na mapadre 6,000. Wawakilishi kutoka zaidi ya nchi 100 nao wamehudhuria wakiwemo marais 24.
article-2614241-1D64A2EA00000578-763_470x711
Rais Robert Mugabe na familia yake
Tukio hilo ni kubwa zaidi jijini Vatican tangu kuchaguliwa kwa Papa Francis mwaka jana.
Hizi ni baadhi ya picha.
article-2614241-1D64AEB300000578-564_964x789
Papa Emeritus Benedict XVI, aliyejiuzulu mwaka jana kwa sababu za kiafya alialikwa na Papa Francis lakini hakuwepo kwenye madhabahu
article-2614241-1D64CBA000000578-799_470x726
article-2614241-1D64CBEB00000578-526_964x710
article-2614241-1D64F69600000578-294_964x626
article-2614241-1D646A2D00000578-173_964x664
article-2614241-1D647A9900000578-1_964x658

 

Post a Comment

أحدث أقدم