Snura alazwa hospitali kutokana na matatizo ya presha .


snura2
Msanii wa filamu na muziki nchini, Snura Mushi amelazwa katika hospitali moja iliyoopo eneo la Kinondoni kutokana na matatizo ya presha ambayo yameanza kumsumbua tangu jana usiku.
Akizungumza na 255 ndani ya XXL ya Clouds FM, meneja wa Snura,HK amesema kuwa Snura bado yupo hospitali baada ya kuzidiwa tena leo asubuhi.
“Ni kweli toka jana usiku manake toka last week, alikuwa kwenye show amerudi vizuri,lakini tangu jana usiku amezidiwa kama saa nne nane saa tisa,usiku sana nikapigiwa simu, yeye anaishi around maeneo ya komakoma hapo na mimi naishi around mitaa ya studio,kwahiyo kama hatua kumi na mbili to ishirini na nne hivi nimefika kwake, nikamchukua nikampeleka hospitali amerudi, lakini sasa hivi tena kidogo hali imeharibika tena kwahiyo tumemrudisha tena hospitalo amelazwa. Ni masuala ya presha kwa mujibu wa daktari tulipozungumza naye, presha ndio linalozingua ,so far sasa hivi anaendelea vizuri kidogo,” alisema HK.

Post a Comment

أحدث أقدم