Ukiwa chuoni ni wakati mzuri wa kuanza biashara

black-female-student
0
Wewe kama mwanafunzi una vitu vingi vya kufanya, masomo, mitihani, kufurahi pamoja na wenzako,  ni ngumu kuanza kitu kingine ukiongezea kwenye masomo. Si kana kwamba kuanza biashara ukiwa chuoni ni rahisi ila inakusaidia kuweka msingi wa kibiashara kama unataka kuendeleza taaluma yako ya biashara. Ukiwa chuoni unatengeneza mtandao wa watu ambao utawatumia baadaye, utashirikiana nao na vile vile kujiimarisha kifedha.
1. Wanafunzi hutoa huduma bora na kwa bei poa kabisa
Chuoni ni sehemu ambayo kila mtu anajifunza, uko darasani na watu walewale kila wakati. Hivyo unapokaribia kumaliza una watu ambao unawaamini na unajua uwezo wao wa kufanya kitu fulani hivyo unawatumia kirahisi au kwa bei nafuu kuliko ungetafuta mtu ambaye hayupo chuoni mwenye uwezo kama huo huo. Wengine wana uwezo wa kukusaidia bure kimawazo hata kufanya baaadhi ya mambo wakati wewe ndo unaijenga hiyo biashara. Hii inakusaidia kuendelea kujifunza pamoja nao na kujenga team hivyo kupunguza gharama za mishahara.
2. Fursa ya kifedha, zaidi ya vile unavyojua!
Tunaishi kwenye ulimwengu wa kunywa pombe na anasa mbalimbali, mitindo tofauti tofauti ya mavazi n.k . Hivyo ukitengeneza wazo lako na ukaamua kupunguza matumizi yasiyokuwa ya lazima unajikuta una mtaji wa kuanza kitu kidogo hapo hapo ulipo. Kama unasomeshwa au kupewa mkopo na serikali unakuwa na uwezo wa kubana matumizi na kufanya kitu cha tofauti, jaribu kuangalia wanafunzi wenzako wanavutiwa na nini kila siku, au ni kitu gani ambacho wanakilipia kila siku na kama unaweza kupata kwa bei rahisi na wewe ukatengeneza faida hapo hapo. Uko eneo la soko ambalo haliingiliwi sana kuliko mtaani ambako ushindani ni mkubwa.
3. Unapata ushauri wa bure kutoka kwa wataalamu
Kila mfanyabiashara ambaye alianza akiwa mdogo atakwambia umuhimu wa kuwa na mtu wa kukushauri. Hivyo ukiingia kwenye ulimwengu wa kawaida tofauti na chuo unataingia kwenye biashara yenye matatizo mengi na ushindani mkubwa huku ukikosha washauri wazuri. Bali unapokuwa chuoni washauri wengi hupenda kutoa hizo huduma bure kwa wanafunzi ili kujitangaza na kusaidia wanafunzi kwa namna moja ama nyingine. Usipuuzie hao watu maana utakapotoka chuoni inakuwa ni vigumu kuwapata.
4. Shida sio kushindwa
Sio mara zote biashara zinafanikiwa, ila unapoanza mapema na huku unaendelea na masomo madhara yake sio makubwa sana kuliko ukiwa nyumbani unafanya biashara hiyo hiyo halafu ikakushinda. Unapoendelea kujifunza unatengeneza taaluma yako ya baadaye kibiashara. Watu wengi watategemea ushindwe, ila kushindwa huko kunakuongezea uzoefu wa kufanya na kuepuka makosa baadaye. Unahitaji ubunifu na kutokukata tamaa pale mambo yanapokuwa hayaendi vizuri.
5. Tengeneza cheo cha kazi unachotaka wewe
Unapoanza kufanya biashara yako , wewe ndio msemaji wa mwisho. Ungependa watu wakutambue kama nani kwenye biashara yako? Lakini inakupa kujitengenezea kazi unayoitaka hasa katika maisha yako, ambayo ungeamua kujiajiri ingekutumia muda mrefu kuja kuifikia.
6. Tafuta kitu unachokitaka
Watu wengi hukimbilia biashara baada ya kumaliza chuo bila kuwa na elimu yeyote au ufahamu wa mambo ya biashara. Kitu ambacho huwafanya kupoteza fedha nyingi na muda, hivyo unapokuwa chuoni jifunze kupitia mafunzo madogo madogo yanayohusu biashara na ufanyie utafiki na mazoezi namna ya kufanya hizo biashara. Ili utakapotoka chuoni ujue ni jambo gani hasa unataka kuliendeleza kibiashra baada ya kujifunza na kujaribu aina mbalimbali za biashara ukiwa chuoni. Hivyo utajikuta unatengeneza taaluma ambayo ndio yatakuwa maisha yako hapo mbeleni.

Post a Comment

أحدث أقدم