Askari aliyefika katika tukio la kifo cha Tupac mwaka 1996 Afunguka na Kusema Haya

Kwa mara ya kwanza tangu kifo cha Rapper Tupac Omar Shakur 1996, polisi aliefika katika tukio dakika chache kabla ya Tupac kufariki kufariki amesema alichokiongea Tupac.

Katika interview na Vegas Seven hivi karibuni, polisi ofisa wa kwanza kufika katika tukio la kifo cha Tupac 1996 ameongea kuhusu maneno ya mwisho yaliyotolewa na Tupac kabla ya kufariki.
Chris Carroll, ofisa wa zamani wa kitengo cha Las Vegas Metropolitan amesema kuwa alipokea simu juu ya tukio la risasi lililotokea karibu na makutano ya Flamingo na Koval mida ya saa 11:15 usiku ambapo alikuwa mwenyewe.
Kutokana na maelezo ya Carroll alipofika katika eneo la tukio na kujaribu kumtaka Tupac kumtaja aliempiga risasi, Tupac alikuwa busy kumkalipia Suge Knight 
"Ninamuangalia Tupac, nae anajaribu kumkalipia Suge , na nnamuuliza, nani amekupiga risasi? nini kimetokea? nani kafanya hivi?, lakini alikuwa akiinipuuzia.alikuwa akiniangalia hapa na pale, lakini anajaribu kumkalipia Suge 
Nikaendelea kumuuliza tena na tena, nani kafanya hivi? nani kakupiga risasi? na akaendelea kunipuuzia, kisha nikaona katika uso wake, katika movement zake, ghafla akabadilika, akaacha kuhangaika na kuanza kuongea bila ushirikiano akisema "niko katika amani" kitu kama hicho, hibyo tu"

Carroll  baadae alielezea maneno ya mwisho aliyoyasema Tupac kabla ya kuanza kukukuruka na kuzimia.
"Aliniangalia na kuvuta pumzi kujaribu kutoa maneno, na akafungua mdomo wake nikidhani ntapata ushirikiano wake, lakini maneno yaliyotoka ni F*** You."

Post a Comment

أحدث أقدم