CIARA na FUTURE wapata mtoto wakiume.

Ciara, Future
Mwanamziki “Ciara Princess Harris” mwenye umri wa miaka 28 amejifungua mtoto wa kiume siku ya jumatatu May 19, Mtoto huyo ambae babake yake ni msanii “Future” ambapo wasanii hao wamekuwa wapenzi kwa muda kidogo. Ciara aliweka picha za mwanae kwenye instagram ikionyesha mkono wa mwanae mchanga kuonyesha kuwa ameshazaliwa. Ciara aliweka wazi ujauzito wake mwezi wa January kwenye The View na kuzungumzia ni jinsi gani alikuwa hawezi kusubiri kupata mtoto huyo ambae kwa sasa ameshakuja duniani. Hii ni kama vile Beyonce alivyofanya wakati anatangaza ujauzito wake soon baada ya kuwa Blue Ivy yupo njiani.
“Nayvadius D. Wilburn” aka Future, 30, alitabiri wakati mahojiano kwenye radio moja huko nchini Uingereza kwamba alikuwa anategemea mtoto huyo kuwa wa kiume. Ciara na Future walitangaza engagement yao mwezi wa October baada ya kuwa katika uchumba wa miezi tisa, Future alimvalisha Ciara pete ya diamond katika weekend ya birthday yake na kufunga pingu za maisha. Future akiwa ni baba wa watoto wawili na sasa ameongeza wa tatu na mkewe mwanadada Ciara.

Post a Comment

Previous Post Next Post