Mwanamziki “Ciara 
Princess Harris” mwenye umri wa miaka 28 amejifungua mtoto wa kiume siku
 ya jumatatu May 19, Mtoto huyo ambae babake yake ni msanii “Future” 
ambapo wasanii hao wamekuwa wapenzi kwa 
muda kidogo. Ciara aliweka picha za mwanae kwenye instagram ikionyesha 
mkono wa mwanae mchanga kuonyesha kuwa ameshazaliwa. Ciara aliweka wazi 
ujauzito wake mwezi wa January kwenye The View na kuzungumzia ni jinsi 
gani alikuwa hawezi kusubiri kupata mtoto huyo ambae kwa sasa ameshakuja
 duniani. Hii ni kama vile Beyonce alivyofanya wakati anatangaza 
ujauzito wake soon baada ya kuwa Blue Ivy yupo njiani.
“Nayvadius D. Wilburn” aka Future, 30, alitabiri wakati mahojiano 
kwenye radio moja huko nchini Uingereza kwamba alikuwa anategemea mtoto 
huyo kuwa wa kiume. Ciara na Future walitangaza engagement yao mwezi wa 
October baada ya kuwa katika uchumba wa miezi tisa, Future alimvalisha 
Ciara pete ya diamond katika weekend ya birthday yake na kufunga pingu 
za maisha. Future akiwa ni baba wa watoto wawili na sasa ameongeza wa 
tatu na mkewe mwanadada Ciara. 
 
 
 
 
  
 
 
 
 
إرسال تعليق