Fid Q na Mwana FA kusubiri ‘Mfalme’ apite, ni ile Collabo iliyohaidiwa na FA wakati wa tuzo za KTMA


Jumamosi iliyopita furaha iliwajaa mashabiki wengi wa Fid Q akiwemo Mwana FA ambaye alimsindikiza Fareed Kubanda jukwaani kupokea tuzo yake ya pili, na wakiwa jukwaani Mwana FA alizungumza kwa niaba yake na kutoa ahadi kuwa kesho yake wangeingia studio kurekodi ngoma.

FID na FA

Hadi sasa Binamu pamoja na Fid Q hawajafanikiwa kuingia studio kama walivyahidi na sababu zilizotolewa na FA ni kuwa wameamua kuipa muda single mpya ‘Mfalme’, ambayo imeonekana kuwa gumzo toka alivyoi-perform Jumamosi kwenye tuzo za Kili na kuitambulisha rasmi Jumatatu wiki hii.

“Bado hatujakaa sawa na Fid kauli yake anasema kwamba hii ‘Mfalme’ ina muda sana hebu tuchukue muda wetu wa kutosha kurekodi ngoma nyingine kali, kwasababu hii Mfalme iko sana kwenye airwaves”. Alisema Mwana FA kupitia Kwetu Flevah ya Magic Fm Jumatano wiki hii.

Post a Comment

أحدث أقدم