Dar es Salaam.Tangu ugonjwa wa homa ya dengue
uibuke mkoani Dar es Salaam na baadaye maeneo mengine ya nchi, wananchi
wamekuwa wakijiuliza maswali mengi yenye utata ambayo sasa yamepata
majibu ya wataalamu.
1. Kwa nini mbu wengine wakiwamo wanaoambukiza malaria hawawezi kuambukiza dengue?
Mtafiti wa tabia za mbu kutoka Taasisi ya Afya ya
Ifakara (IHI), Dk Nicholaus Govela alisema mbu anayeambukiza homa ya
dengue, Aedes Egypti, hawezi kubeba vimelea vya malaria wala yule
anayeambukiza malaria hawezi kuambukiza dengue kutokana na maumbile yao.
Dk Govela alisema fiziolojia ya mwili wa mbu haiwezi kuruhusu Aedes Egypti kubeba virusi vya mbu mwingine.
“Ndiyo maana mbu hawezi kuambukiza Virusi vya Ukimwi,” alisema.
2. Kwa nini mbu wa dengue huuma mchana?
Dk Govela alisema suala hilo bado linahitaji
utafiti zaidi kwa sababu kati ya aina tatu za mbu wanaosababisha dengue,
hakuna utafiti uliofanyika kujua tabia zao wote.
Aina hizo ni Aedes Egypti, Aedes Albokictus na Aedes Africaans.
Alibainisha kuwa katika tafiti zinazofanyika, IHI
iliwahi kubainika kuwa Aedes African ambaye pia anaambukiza dengue huuma
usiku.
Alisema wengi wanamwelezea mbu huyu kwa
kumlinganisha na tabia za mbu wa Japan, China na America ya Kusini
lakini inawezekana huyu aliyepo hapa ni mpya tofauti na wa nchi za nje.
3. Je, dawa inayopulizwa inafaa kuwaangamiza?
Dk Govela alisema inawezekana ndiyo au hapana,
lazima hili pia lifanyiwe utafiti kwa kuwa upo uwezekano wa mbu hawa
kujenga usugu wa dawa kwa kuwa wamekuwapo nchini kwa miaka mingi.
Soma Zaidi
Soma Zaidi
Post a Comment