Hivi ndivyo Justin Bieber, azungumzia Kesi yake ya wizi. ‘Ukweli Utakuweka Huru’

url
Siku moja baada yakutimiza miaka 20, Justin ambae ameshitakiwa kwa kesi ya wizi mjini Los Angeles Califonia ameandika kupitia Twitter ujumbe unaomwesha kwamba yeye  hana hatia na mashtaka hayo. Mwanamke mmoja  ameshtaki kwamba Bieber alitaka kumwibia simu yake jumatatu usiku, pale Sherman Oaks Castle Park kwenye mji wa L.A.’s San Fernando Valley. Siku ya jumatano asubuhi, katika kituo cha polisi kimoja mjini L.A wamewaeleza waandishi wa habari kwamba Bieber ataachiliwa kwa dhamana mpaka uchunguzi zaidi utakavyomalizika.
Wakichukua maneno aliyoandika kwenye Twitter, si rahisi kuyaamini maana msanii huyu ameshajiingiza katika matatizo mengi ya kuvunja sheria. Beiber alishitakiwa  na kesi  yakuendesha gari lake na leseni iliyopita mda wake kwenye mji wa Miami, vile vile kipindi cha nyuma pia alishitakiwa na kesi ya kumvamia jirani yake na na kugonga gari kwa nyuma.
Sasa kuna mwanamke mmoja aliyekuwapo usiku ule wa wizi,amewapigia TMZ Live nakuelezea alichokiona. “Bieber hakushika mfuko wala mkoba wake, Bieber hakumwongelesha jambo lolote bali yule mama alikuwa aking’ang’ania kuchukuwa picha na msanii huyo. Bieber alikataa ila ule mama aling’ang’ania mpaka Iliwabidi walinzi wake wamwondoe yule mama maana alikuwa mkaidi sana. Mtoto wake wa miaka 13 alibakia akilia huku akiwa ameshika simu yake mkononi ila Bieber hakujaribu kumwibia au kunyang’anya .

Post a Comment

Previous Post Next Post