
Wasanii mbalimbali wakiwa katika
mahojiano ya redio ili kuitangaza ziara ya muziki ya Kilimanjaro
(kilimanjaro Music Tour) ambapo show kubwa itafanyika katika Chuo Cha
Ushirika Moshi kwa udhamini wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.wasanii
hao walitembelea Kili Fm na Moshi Fm. Zaidi ya wasanii kumi maarufu
nchini watatoa burudani ya aina yake katika show itakayoanza saa nne
asubuhi hadi saa kumi na mbili jioni.Huu ni mwanzo wa show takriban kumi
zitakazofanyika katika mikoa mbalimbali.

إرسال تعليق