
Watu wasiopungua 37 wameuawa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo katika hujuma ambayo imetajwa kuwa ni ulipizaji kisasi kufuatia
wizi wa ng'ombe.
Tukio hilo limejiri jana Jumamosi katika kijiji kimoja mkoani Kivu
Kaskazini na imearifiwa kuwa kati ya waliopoteza maisha ni mwanamke na
watoto ambao walipigwa risasi na kudungwa visi au kuchomwa moto ndani ya
nyumba zao.
Baadhi pia wameuawa wakiwa ndani ya kanisa kijijini hapo walipokuwa wakikimbilia hifadhi.
Waathirika wote wa hujuma hiyo ni wa kabila la Bafuliru.
Waathirika wote wa hujuma hiyo ni wa kabila la Bafuliru.
Bado haijabainika ni nani hasa aliyetekeleza hujuma hiyo lakini kwa muda
sasa kumekuwepo na mzozo baina ya watu wa kabila la Bafuliru na
Warundi wanaoishi katika eneo hilo.
Gavana wa Kivu Kusini Marcellin Cishambo amethibitisha kuwa mgogoro huo
ulikuwa wa mifugo na kuongeza kuwa tatizo kubwa ni kwamba karibu kila
mtu ana silaha katika eneo hilo.
Eneo la mashariki mwa DRC limekuwa likikumbwa na machafuko ya mara kwa mara tokea mwaka 1998.
Source: kiswahili.irib.ir
إرسال تعليق