Waziri
 wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (kulia) 
akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Haak Neel Production (T) Limited Bw. 
Emmanuel Mahendeka wakati wa hafla ya uzinduzi wa siku ya Msanii 
itakayoadhimishwa tarehe 25 Oktoba,Siku ya Msanii inaratibiwa kwa 
ushirikiano baina ya Baraza la Sanaa la Taifa BASATA na Kampuni hii ya 
Haak Neel Production. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara ya 
Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga na Kaimu Katibu 
Mtendaji wa BASATA  Bw. Godfrey Mungereza  
 
 
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba 
Nkinga akiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa hafla 
ya uzinduzi wa siku ya Msanii itakayoadhimishwa tarehe 25 Oktoba, Hafla 
hii imefanyika mwishoni mwa wiki hii katika Hotel ya Sea Cliff jijini 
Dar es Salaam.  
 
 
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba 
Nkinga akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Haak Neel Production (T) 
Limited Bw. Emmanuel Mahendeka wakati wa hafla ya uzinduzi wa siku ya 
Msanii,mapema wikiendi hii, jijini, katikati ni Mkurugenzi wa Maendeleo 
ya Utamaduni Profesa Hermas Mwansoko na Kaimu Katibu wa BASATA Bw. 
Godfrey Lubejo Mungereza. 
 
 
Waziri
 wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara 
(katikati) akishiriki kuwakumbuka  Wasanii waliotangulia mbeleza za 
haki, kabla ya kuendelea na hafla ya uzinduzi wa Siku ya Msaanii 
itakayokuwa inaadhimishwa tarehe 25 Oktoba kila mwaka.Kutoka kushoto ni 
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Profesa Hermas Mwansoko, Katibu 
Mkuu wa Wizara ya Habari Bibi. Sihaba Nkinga, Mkurugenzi Mkuu wa Haak 
Neel Production Bw. Emmanuel Mahendeka na Kaimu Katibu Mtendaji wa 
BASATA Bw. Godfrey Mungereza. 
 
 
Kaimu
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) akielezea kwa 
ufupi histori ya Siku ya Msanii wakati wa hafla ya uzinduzi wa Siku hiyo
 itakayokuwa ikiadhimishwa tarehe 25 Oktoba kila mwaka. 
 
Mkurugenzi
 Mkuu wa Kampuni ya Haak Neel Production (T) Ltd Bw. Emmanuel Mahendeka 
 akizungumza na wadau wa sanaa wakati wa hafla ya uzinduzi wa Siku ya 
Msaanii iliyozinduliwa mapema wikiendi hii jijini Dar es Salaam. 
 
 
Waziri
 wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akipiga 
Gitaa wakati wa hafla ya uzinduzi wa Siku ya Msanii itakayokuwa 
ikiadhimishwa tarehe 25 Oktoba kila mwaka 
 
 
Mkurugenzi
 wa Kituo cha Utamaduni wa India hapa nchini Bibi. Chitra Suresh (wapili
 kutoka kulia) akifuatilia baadhi ya kazi za wasanii wakati wa hafla ya 
uzinduzi wa Siku ya Msanii mapema wikiendi hii jijini Dar es Salaam. 
 
 
Mwanamitindo
 mkongwe Asiah Idarius wa kwanza akiwa na baadhi ya wanamitindo wake 
wakati wa hafla ya uzinduzi wa hafla Siku ya Msanii mapema wikiendi hii. 
 
 
Wasanii
 wa Kikundi cha Ngoma kutoka Dodoma wakitumbuiza wakati wa hafla ya 
uzinduzi wa Siku ya Msaani mapema wikiendi hii jijini Dar es Salaam. 
 
 
Waziri
 wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akipokea
 zawadi ya gauni kutoka kwa mbunifu  wa mavazi na Mwanamitindo Asiah 
Idarius(katikati) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Siku ya Msaani mapema 
wikiendi hii jijini Dar es Salaam. 
 
 
Waziri
 wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (mwenye 
koti jeupe) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bibi Sihaba Nkinga  wakiwa 
katika picha ya pamoja na wadau wa Sanaa wakati wa hafla uzinduzi wa 
Siku ya Msanii iliyofanyika mapema wikiendi hii jijini Dar es Salaam.
إرسال تعليق