Wizara ya afya na ustawi wa jamii imeifungia hospitali ya St Harry
iliopo katikati ya mji wa Morogoro kutokana na kutoa huduma za afya
katika jengo ambalo halina viwango vya kutoa huduma za matibabu kwa
wagonjwa
Mganga mkuu wa mkoa wa morogoro dr godfrey
mtei na mganga mkuu wa manispaa ya morogoro Dr Abraham Mahizo ambao
wameongoza zoezi la kufunga hospitali hiyo wamesema wamefikiaumamuzi
huo katika kutekeleza maagizo ya wizara ya afya waliyoyatoa baada ya
kufanya ukaguzi na kubaini kuwa hospitali hiyo haina vigezo vya kutoa
huduma kwa wagonjwa ingawa walipewa muda wa miezi kadhaa kuhamia katika
jengo lao jipya lakini bado wamekiuka utaratibu na kuendelea kutoa
huduma za afya katika hospitali hiyo.
Nae mmoja wa wasimamizi wa hosipitali hiyo
inamilikiwa na kanisa la international Karismatic church of Tanzania
ICT, Mandia Kerem amesema wanasikitishwa na hatua ya wizara ya afya
kufungia hospitali hiyo kwani kunamzunguzo yaliokuwa yakiendelea na
kwamba kufungwa huko kutaathiri na kusababisha usumbufu kwa wagonjwa
wanaotegemea hospitali hiyo kupata matibabu huku wakionekana
kuwaelekeza wagonjwa waliofika hospitalini hapo kuhamia katika jengo
lao jipya .
إرسال تعليق