 Mjumbe
 wa  Bunge Maalum la Katiba, ambaye pia ni mwanasiasa mkongwe nchini , 
Mzee Kingunge Ngomabale Mwiru amesema  Katiba bora ni ile 
itakayozingatia  historia  mafanikio ya  miaka 50 iliyopita na Muungano 
imara.
Mjumbe
 wa  Bunge Maalum la Katiba, ambaye pia ni mwanasiasa mkongwe nchini , 
Mzee Kingunge Ngomabale Mwiru amesema  Katiba bora ni ile 
itakayozingatia  historia  mafanikio ya  miaka 50 iliyopita na Muungano 
imara.
Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Mzee Kingunge wakati akichangia  katika mjadala wa Bunge hilo  juu ya uwasilishaji
 wa taarifa  za Kamati Namba Moja hadi Kamati Namba Kumi na Mbili za 
Bunge hilo kuhusu uhakiki wa Rasimu  ya Katiba  iliyopendekezwa.
 Aidha Mzee Kingunge amesema  wameondosha mapendekezo ambayo yanataka kusambaratisha muungano ili uweze kuwa imara.   
 Mzee
 Kingunge aliyataja mambo matatu ambayo yatazingatia Katiba  bora kuwa 
ni  ni ile itakayoimarisha historia ya mafanikio ya miaka 50 iliyopita, 
inayopunguza  na kuondoa kero mbalimbali za msingi.
 Aliongeza
  kuwa tatu ni “Lazima Katiba  Mpya iingize mambo  ambayo yataimarisha 
nafasi za wananchi mfano wakulima , wafugaji, wavuvi, wasanii na 
wachimbaji wadogo… Tanzania haitakuwa  kama ilivyokuwa huko nyuma baada 
ya mkutano huu.
 “ Kwa sababu makundi yote yote yamekutana hapa kuzungumzia maslahi yao na hatma yao,” alisema Mzee Kingunge.
 Mzee Kingunge alisema mawazo yaliyotolewa na ni ushindi mkubwa, kazi iliyobaki ni kupitisha.
 “Kazi  hii si ndogo ni kubwa…kwani  kuna  zogo 
, lakini tumevulia napenda iandikwe kwa wino wa dhahabu kama ilivyo hapa ndani,” alisisitiza.    
 Mwanasiasa
 huyo alifafanua  kuwa  Katiba ni maridhiano, hivyo anajua wakubwa 
wataendelea kuzungumza, hivyo katika hilo ni vizuri wakawa waangalifu.
“ Tuifanye kazi hii kwa unyenyekevu, wananchi  wanangoja Katiba bora,” alisema.
Kwa
 upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalum la 
Katiba,Mhe. Andrew Chenge alisema wakati akihitimisha mjadala huo, si 
rahisi kuweka mambo yote kama yalivyotolewa na baadhi ya wajumbe wa 
Bunge hilo, bali itachukua yale ya msingi mengine yatazingatiwa  katika 
Sheria za Nchi.
Aliwaasa
 Watanzania kuisoma Rasimu ya Katiba Mpya  iliyopendekezwa na  Tume ya 
Mabadiliko ya Katiba  na ile Rasimu ya  Katiba Mpya iliyopendekezwa na 
Bunge hilo.
Ninyi ndio  mtakaoamua ukweli uko wapi?  Tumeboresha hakuna kazi ya kuweka koma tumekuja kuandika Katiba ya Watanzania.
Mhe. Chenge alisema  Kamati yake ni wajumbe ambao ni hazina kwa Tanzania.
Kwa
 upande wake, mjumbe wa Bunge hilo, Mhe. Profesa Mark Mwandosya alisema 
 kazi iliyofanywa na Bunge hilo imefanywa kwa uadilifu, hivyo 
wamezingatia Rasimu ya Katiba Mpya  ya  Tume na wameboresha kwa 
kuzingatia maslahi ya wananchi. 
Post a Comment