NHIF YAKAMATA WATU WANAOTUMIA KADI ZA BIMA YA AFYA KINYUME NA UTARATIBU KATIKA HOSPITALI YA REGENCY

1 
Bw. Julius Mziray mkaguzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) akizungumza na waandishi wa habari katika hospitali ya Regency ya jijini Dar es salaam. Baada ya kumkamata mtu mmoja anayetuhumiwa kutumia kadi ya bima ya afya yenye namba 02-HCTP1801 ambayo  inamilikiwa na Bw. Terry J. Maona kinyume na utaratibu , Mtu huyo alikamatwa jana katika hospitali hiyo wakati akitaka kufanya vipimo vya (CityScan), ndipo mmoja wa wafanyakazi wa hospitali hiyo alipogundua na kupiga simu makao makuu ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)  kuwataarifu kuhusiana na tukio hilo, ambapo maofisa walifika na kukamata nyaraka hizo huku mgonjwa akitokomea kusikojulikana baada ya kugundulika, Bw. Julius Mziray amewaasa wamiliki wa kadi za Bima ya Afya kutozitumia watu tofauti badala yake zitumie kwa  wahusika walioorodheshwa katika bima hiyo tu   Jambo ambalo kuwaigiza katika mikono ya sheria na kupata adhabu kali. 2 
Bw. Julius Mziray mkaguzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF akiwasomea waandishi wa habari maelezo yaliomo katika nyaraka hizo  
 3Baadhi ya wgonjwa mbalimbali wakisubiri huduma katika hospitali hiyo 
 4Baadhi ya wgonjwa mbalimbali wakipata  huduma katika hospitali hiyo

Post a Comment

أحدث أقدم