
Meneja
 wa mawasiliano wa Tigo Bw. John Wanyancha akiongea na waandishi wa 
habari (hawapo pichani), kutangaza udhamini wa kampuni ya Tigo safari 
ya  timu ya Taifa ya watoto waendesha mitumbwi inayoelekea nchini 
Morocco kushiriki mashindanoya wakimbiza mitumbwi mwezi ujao.
Na Mwandishi wetu
 Tigo
 Tanzania  imetangaza udhamini wake kwa timu ya taifa ya watoto wadogo 
waendesha mitumbwi, timu ambayo inaundwa na mabaharia watoto 10 
waliochaguliwa na shirikisho la mitumbwi midogo ya watoto Tanzania 
(TODA). Timu hii ya Taifa itashiriki mashindano ya 12 ya wakimbiza 
mitumbwi wadogo Afrika yatakayofanyika Agadir, nchini Morocco kuanzia 
tarehe 10 mpaka 18 Oktoba 2014.
Kukimbiza
 chombo hiki ni zoezi la kuendesha mtumbwi mdogo, kwa kawaida si zaidi 
ya urefu wa mita 6. Boti hii ya watoto wadogo ina urefu wa mita 2 na 
inafaa kwa ajili ya watoto wa chini ya umri wa miaka 16.
Meneja
 wa Mawasiliano wa Tigo John Wanyancha alisema kuwa udhamini huu wa Tigo
 ni sambamba na dhamira ya kampuni hiyo kuwekeza katika kukuza vipaji 
vya wanamichezo nchini kuanzia wenye umri mdogo.
“Michezo
 inatambuliwa kama jambo muhimu si tu katika maendeleo ya vijana lakini 
pia katika kuunganisha vijana kutoka asili tofauti tofauti. Ni njia 
muhimu sana katika kuongeza kujiamini na kujifunza ujuzi upya. Ni 
makusudio yetu kuendeleza jitihada hizi za kuhamasisha mazingira ya 
michezo hapa Tanzania,” alisema Wanyancha.
Aliongeza,
 “Tunaamini katika uwezo wa mchezo kuwawezesha vijana kutimiza malengo  
yao muhimu maishani. Sekta ya michezo inajenga fursa nyingi za ajira kwa
 vijana ambao wanatamani kutumia vipaji na ujuzi wao  ili kuleta 
mabadiliko chanya katika maisha yao.”
Mwakilishi
 wa nchi wa Shirikisho la mitumbwi midogo ya watoto Tanzania (TODA), 
Nelly Coelho, alieleza kuwa uendeshaji wa mitumbwi hii ya watoto ni 
mahsusi kwa ajili ya mabaharia vijana wenye umri kati ya miaka 8-15.

Meneja
 wa mawasiliano wa Tigo Bw. John Wanyancha akipiga picha ya pamoja na 
Timu ya Taifa ya watoto mabaharia waliochaguliwa na shirikisho la 
mitumbwi midogo ya watoto Tanzania(TODA) itakayoshiriki mashindano ya 
wakimbiza mitumbwi yatayofanyika Agadir Morocco kuanzia tarehe 10 hadi 
18 oktoba mwaka huu, Tigo ndio mdhamini wa safari hiyo.
Aliongeza
 kusema, “Mabaharia waliofuzu wamekuwa wakipewa mafunzo kwenye ukingo wa
 bahari wa Msasani kutoka chama cha wamiliki wa majahazi, Dar es Salaam.
 Wengi wao walishawahi kushiriki katika mashindano mawili yaliyopita ya 
Afrika chini ya ufadhili wa Shirikisho la Mabaharia kwa kushirikiana kwa
 msaada wa vifaa vilivyotolewa na chama cha wenye Majahazi Dar es 
Salaam, ambao TODA inatoa shukrani nyingi kwao .”
Msaada
 wa Tigo umekuja kwa wakati mwafaka ambapo TODA ina mikakati ya  
kutangaza mbio za vyombo vya majini kama njia ya kuendeleza vijana. 
Mwakilishi wa TODA nchini amewashukuru Tigo kwa msaada huo na kuhimiza 
ushirikiano huo uwe endelevu.
Mashindano
 ya 12 ya watoto Afrika yameratibiwa kwa ushirikiano wa Shirikisho la 
Royale Marocaine de Voile na Shirikisho la kimataifa la Mitumbwi ya 
Watoto (TODA). Mashindano yatazileta pamoja nchi 13 barani Afrika ili 
kushindana kwa ajili ya michuano hiyo. Kila nchi mwanachama katika 
Afrika watapeleka mabaharia wapatao 10, waliofuzu katika majaribio ya 
Taifa. Pia TODA wanahamasisha kuwa kati ya hao mabaharia 10 katika timu 
angalau 3 wawe mabaharia wa kike ili kuhamasisha ukuaji wa vikosi kazi 
kwa wasichana. Hii ni mara ya tatu kwa Tanzania kupeleka wawakilishi 
wake kwenye tukio hili la kila mwaka kupitia Shirikisho la Mitumbwi 
midogo Tanzania (TODA). Tukio hilo lilifanyika mwaka 2005 na 2012, 
kwenye chama cha wamiliki wa Majahazi Dar es Salaam. Watoto watakaoenda 
nchini Morocco ni Alexandra Pennanen Kok(13),Savanna Desmarguest(13), 
Casey Deetlefs(12),Said Mkomba(13)
 Hassan Mustafa(14), Vedastus Alphonce(14), Max Pennanen Kok(14), Friso Grolleman(12), Karim Jumanne(11) na Lenno Telemons(12).

Meneja
 wa mawasiliano wa Tigo Bw. John Wanyancha akiongea na Timu ya Taifa ya 
watoto mabaharia waliochaguliwa na shirikisho la mitumbwi midogo ya 
watoto Tanzania(TODA) itakayoshiriki mashindano ya wakimbiza mitumbwi 
yatayofanyika Agadir Morocco kuanzia tarehe 10 hadi 18 oktoba mwaka huu,
 Tigo ndio mdhamini wa safari hiyo.

Watoto mabahria wakiwa kwenye mazoezi na mitumbwi yao maeneo ya slipway kujiandaa na safari ya nchini Morocco mwezi ujao.

Mtoto
 baharia Max Pennanen Kok akionesha uhodari wake wa kuendesha mtumbwi 
kwenye fukwe za bahari ya Hindi maeneo ya Yatch club mtoto huyo ni mmoja
 ya watoto kumi watakaoshiriki mashindano ya wakimbiza mitumbwi nchin 
Morocco mwezi ujao, Tigo ni wadhamini wa safari hiyo.
إرسال تعليق