Mamia
 ya waandamanaj wa Hong Kong wamezingirwa na Askari polisi wanaowataka 
kusitisha maandamano na mkusanyiko wao karibu na ofisi za Makao makuu ya
 serikali.
Waratibu wa maandamano hayo wamekaidi amri hiyo na 
kuwataka watu wengine zaidi kujitokeza ili kuwaunga mkono katika madai 
yao ya kuitaka China iwaachie uhuru wa kumchagua kiongozi wao katika 
uchaguzi ujao wa mwaka 2017.
Kiongozi wa Mamlaka ya Hong Kong C Y 
Leung amesema serikali yake imesikiliza na kuzingatia madai ya 
waandamani lakini inapingana na mpango wao wa kujitenga.
 ‘’Mimi 
na serikali yangu tutazingatia sheria za msingi na uamuzi unaostahili wa
 NPCSC,tutajaribu juhudi zote kutekeleza uchaguzi wa kiongozi mkuu kwa 
kila anayestahili kupiga kura atafanya hivyo mwaka 2017. Serikali 
itaanzisha hatua inayofuata ya majadiliano kuboresha katiba hivi hivi 
karibuni. Inasihi sekta mbalimbali za jamii kushiriki katika majadiliano
 yenye mantiki kwa Amani na kwa kufuata sheria, kufikia makubaliano na 
kukubali tofauti pamoja na kuruhusu watu milion tano wenye uhalali wa 
kupiga kura hapa Hong Kong kumchagua kiongozi mkuu mwaka 2017 mtu mmoja 
kura moja’' amesema Leung Chung-ying.
‘mimi na serikali yangu 
tumekuwa wasikivu kwa raia na tumejitolea kudumisha jamii yote. Wananchi
 wanatakiwa kutoa wanayoyahitaji kwa Amani, mantiki na kisheria, na 
kuheshimu na kuzingatia mitazamo mbalimbali katika jamii. Serikali ya 
SAR ya Hongkong imeazimia kupinga utawala usio wa kisheria wa ofisi za 
serikali kuu au makao makuu ya wilaya ‘utawala wa seriakli kuu’’. Polisi
 wanajitambua kukabiliana na hali kwa wakati kwakuzingatia sheria’’ 
Ameongeza

Post a Comment