Gadner G Habash amejiunga na kituo cha redio cha EFM 93.7 Dar es Salaam.
Gadner (kulia) akiwa na Lamar kwenye uzinduzi wa video za Profesa Jay hivi karibuni
Kabla ya hapo, mtangazaji huyo mkongwe alikuwa akiendesha kipindi cha jioni, Maskani cha Times FM.
“Gardner ataendesha kipindi kiitwacho Ubaoni kuanzia
saa tisa alasiri mpaka saa moja kamili jioni kuanzia Jumatatu ya tarehe
03 mwezi wa 11 mwaka huu,” afisa habari wa kituo hicho Kanky Mwaigomole
aliwaambia waandishi wa habari.
Gadner ni miongoni mwa watangazaji wanaoheshimika zaidi nchini na
alijizolea umaarufu zaidi kupitia Clouds FM aliyoitumikia kwa miaka
mingi kabla ya kuondoka.
Post a Comment