Picha ya pamoja mkuu wa Jeshi la Police Nchini Erenest Mangu na
Viongozi wa Mkoa wa Ruvuma aliye simama
kushoto
wa kwanza ni Sheikh Yusufu Kambaulaya
|
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu amewataka
wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi
hilo katika kutokomeza uhalifu.
Alisema pasipo kuwapo na ushirikiano dhana ya polisi jamii haitafanyakazi iliyokusudiwa na
jamii itaishi kwa mashaka.
Kauli hiyo ameitoa Songea hivi karibuni wakati wa wakati wa
chakula cha jioni ikulu ndogo mjini hapa.
Alisema ushirikiano ulioonyeshwa na wadau mbalimbali wakiwemo
viongozi wa Dini ndiko kumewezesha nchi hii kuendelea kuwa na amani.
Aliwataka viongozi kuhubiri amani na utii wa sheria bila shuruti
hivyo kurahisisha kazi ya jeshi hilo kupambana na uhalifu.,
Akishukuru baada ya kukabidhiwa zawadi mbalimbali ikiwamo Kurani
tukufu aliyokabidhiwa na Shehe wa Mkoa wa Ruvuma Yusufu Athumani Kambaulaya alisema:“Ni juu ya kila Mmoja kuendeleza
juhudi za kulinda amani na kuwa msitari wa mbele kushirikiana na Serikali
kupinga uhalifu na kuweza kuwaumbua wale wanao endeleza uovu.”
Aliwataka viongozi wa dini kuwahubiria waumini wao namna bora ya
kuenzi amani ikiwa na pamoja na kuwuambua wahaklifu wa aina zote bila kujali
wadhifa wao katika jamii.
Mchana katika ziara yake mkoani Ruvuma mkuu huyo wa Polisi nchini
alikagua Jengo la Dawati la Jinsia na Watoto Jengo lililo gharimu
shilingi milioni 38.
Jingo hilo ambalo limewezeshwa kwa njia ya msaragambo chini ya
kamati ya uhamasishaji iliyoongozwa na Adamu
Mzuza Nindi limeweza kusaidia wanawake na watoto kuwa na faragha katika
matatizo yanayowakuta.
إرسال تعليق