Kocha mkuu wa Simba, Patrick Phiri.
MWENDO wa
kusuasua tangu kuanza kwa ligi kuu msimu huu, umeanza kuzua hofu kwa
viongozi na wanachama wa kikosi hicho, lakini kocha mkuu, Patrick Phiri
ameibuka na kuweka bayana kinachoimaliza timu hiyo.
Phiri ambaye ameshuhudia kikosi chake kikishindwa kuwika mbele ya
timu za Coastal Union, Polisi Moro na Stand United kikiwa nyumbani
kwenye Uwanja wa Taifa, amefunguka na kutaja ‘mchawi’ mkubwa ni
kujiamini kwa wachezaji kabla ya mchezo, msongo wa mawazo pamoja na
kuandamwa na majeruhi.
Akizungumzia mwenendo wa kikosi chake, Phiri alisema wachezaji wake
wamekuwa na kasumba ya kujiamini kwa kiasi kikubwa, hasa wanapokuwa
wakiongoza, ndiyo maana wamekuwa wakianza kwa kasi na kulisakama lango
pinzani mara nyingi, lakini hujikuta wakimaliza kwa kuchechemea.
Phiri amekiri kuwa kikosi chake kimekuwa kikicheza vyema dakika 50 hadi 60 huku akitaja sababu kuwa ni kujiamini kwa wachezaji.
“Siyo kusema labda wachezaji wetu wanakosa stamina, hapana, ni hali
ya kuridhika na matokeo, hasa timu inapokuwa ikiongoza. Pili, wanakuwa
na ‘stress’ kutoka kwa mashabiki hasa pale timu pinzani inaposawazisha,
wachezaji hujikuta wakicheza kwa presha, jambo ambalo huwaathiri jumla,”
alifunguka Phiri.
Aliongeza kuwa jinamizi la majeruhi kwa kiasi kikubwa limechangia
kuharibu programu zake za kusaka kikosi cha kwanza, huku akilia na Paul
Kiongera na Ivo Mapunda ambao walitarajiwa kuwa msaada mkubwa Simba.
Post a Comment