POLISI
mkoani Arusha inawasaka madereva wawili wa magari mawili ambayo
yalisababisha ajali iliyoua abiria 12 na kujeruhi wengine watatu.
Madereva
hao ni wa basi dogo la abiria aina ya Nissan lenye namba za usajili
T519 BDJ na lori la mafuta aina ya Scania lenye namba za usajili T 582
ACR ambao magari yao yaligongana katika barabara ya Arusha Moshi eneo la
Madira baada ya basi hilo kutaka kuyapita magari mengine bila ya
kuchukua tahadhari na ndipo likakutana uso kwa uso na lori hilo, hivyo
kusababisha ajali iliyoua watu 12, tisa wakifa papo hapo.
Kwa
mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas,
waliokufa na kutambuliwa ni pamoja na Simon Elipokea Ngolenya aliyekuwa
kondakta wa basi dogo, Kundaeli Kaaya aliyekuwa mwalimu shule ya msingi
Ndoomba wilayani Meru na mkewe, Elly Kaaya aliyekuwa mtumishi wa
halmashauri ya Meru, Idara ya Masjala.
Wengine
ni Leticia Ruhangiza ambaye ni Ofisa Elimu ya Watu Wazima katika
halmashauri ya Meru na Zakia Kitunga, ambaye ni mwalimu katika
halmashauri ya Meru.
Kamanda
Sabas alisema maiti saba bado hawajatambuliwa na wako katika chumba cha
kuhifadhi maiti katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru wakisubiri
kutambuliwa, kati ya maiti hao saba wanaume wako wanne na wanawake
watatu.
Majeruhi ni Alfred Nyabi (36), Mariam Aloyce ambao ni wakazi wa Usa River.
Post a Comment