Macho yaelekea kwenye uzinduzi nchini Tanzania!
Kampuni
ya Samsung imezindua toleo jipya la simu zake za Galaxy Note 4 Jijini
Berlin Nchini Ujerumani Septemba 2014. Toleo hilo la teknolojia ya
kisasa katika orodha za simu aina ya Note inazidi kuimarisha kampuni ya
Samsung na kuzidi kufanya vizuri katika soko la simu duniani. Siku ya
tarehe 17 Octoba, 2014 Kampuni ya Samsung ilifanya uzinduzi Mjini wa
Cape Town- Afrika Kusini katika ziara ya Galaxy Note 4 Barani Africa.
Watanzania
wanatarajiwa kupanga mistari katika maduka ya Samsung kushudia toleo
jipya la simu katika familia ya Galaxy Note. Hii inatokana na uzinduzi
mkubwa uliyofanyika Cape Town-Afrika Kusini ambayo ilikua ni ishara ya
upatikanaji wa simu hizi za kisasa katika soko la Bara la Afrika na
Tanzania ikiwemo.
Kutokana na Uzinduzi mkubwa uliofanyika Berlin, simu hii imepata umaarufu mkubwa na kujulikana kama ‘‘muongozi wa mabadiliko katika ulimwengu wa simu (smartphones) za mkononi’’. Galaxy
Note 4 mpya ina kioo kikubwa chenye ubora zaidi wa kuonyesha matukio,
na kalamu (S Pen) ya kipekee inayompa mtumiaji uhuru na uwezo mkubwa wa
kutumia simu hiyo.
Uzinduzi
Barani Afrika Ulihusisha viongozi mbalimbali wa kampuni ya Samsung
duniani akiwemo Mh. Mike Seo Mkurugenzi Mtendaji wa Samsung Electronics
Tanzania, pamoja na mawakala wa Samsung, waandishi wa Habari na
washiriki wengine.
Akiongea kwa hamasa kubwa kuhusu uzinduzi unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni katika soko la Tanzania Mh. Mike Seo alisema ‘‘
Tunatazamia kuleta toleo jipya la Galaxy Note kwa wateja wetu nchini
Tanzania. Kutokana na muunganiko wa Teknologia mpya na maoni kutoka kwa
wateja wetu sasa tunaleta utamaduni wa kalamu na karatasi katika
ulimwengu mpya wa teknologia ya kisasa nchini Tanzania’’
Uingiaji
wa haraka wa simu hii maeneo ya Kusini mwa Jangwa la Sahara ni ishara
kubwa inayoonyesha umuhimu mkubwa wa Africa katika soko la dunia,
kutokana na watumiaji kutambua ukuaji wa teknolojia katika maisha yao.
Hivi karibuni ukuaji na uwezo wa watanzania kwenye soko kunadhihirisha
kuwa hawana haja ya kuendelea kusubiri simu hii kutiririka nchini miezi
kadhaa baada ya kuzinduliwa kwenye mabara jirani kama Asia na Ulaya.
Huitaji wa bidhaa zenye technolojia ya hali ya juu unazidi kuhongezeka
na Samsung imejikita katika kuendeleza uhitaji huo wa Tekinolojia mpya
inayopanda siku hadi siku katika nchi mbalimbali Barani afrika.
Ikifuatia
mafanikio ya matoleo ya Galaxy Note, Duniani kwa ujumla Galaxy Note 4
inakidhi matarajio ya watumiaji. Kampuni ya Samsung ina matarajio
makubwa ya simu hii ya kisasa katika soko la Tanzania na Afrika kwa
ujumla. Simu hii inaakisi kile ambacho kampuni ya Samsung huona kama
mchango muhimu unaotolewa na soko la Afrika katika soko la dunia.
Samsung
inawaahidi watumiaji wake ubora na utofauti wa kipekee kupitia Galaxy
Note 4. Simu hii itapatikana kwa rangi mbali mbali kama Nyeusi, Nyeupe,
Dhahabu, Pinki ikiambatanishwa na kalamu ya simu ambayo huraishisha
matumizi ya simu hiyo.
Wateja
wote wanaweza kujua zaidi kuhusu simu hii kwa kupitia programu ya
Galaxy Note 4 inayopatikana kwenye PlayStore au kutembelea maduka yoyote
yaliyo idhinishwa na Samsung,
Baadhi ya sifa kuu ambazo watumiaji watafurahia kutumia Galaxy Note 4:
Kalamu (S Pen)
Imetengenezwa
kisasa kumfanya mtumiaji kuandika kwa ubora. Uwezo mkubwa unamfanya
mtumiaji kuhisi kama anaandika au kuchora kwenye karatasi. Pia simu hii
ina uwezo wa kupiga picha maandishi na kuugeuza katika maandishi ndani
ya simu.
Kamera
Simu
inakuja na camera ya nyuma yenye uwezo wa MegaPixels 16 na Kamera ya
mbele yenye uwezo wa Megpixels 3.7.Ina uwezo wa kujirekebisha yenyewe
kulingana na hali ya hewa au eneo kutoa picha Nzuri.
Betri
Simu
hii ina uwezo wa kuchaji kuanzia asilimia 0 mpaka 50 kwa dakika 30.
Kama ilivyo kwa simu aina ya Galaxy S5 simu hii pia ina mfumo wa
kutunza chaji ambao unaruhusu kuhifadhi chaji kwaajili ya matumizi ya
muhimu ya simu pale chaji inapoisha kabisa.
Hupunguza kelele
Inampatia mtumiaji uwezo wakuwasiliana kwa urahisi kutokana na uwezo wa simu kupunguza kelele za pembeni.
Ulinzi
Ina ulinzi wa alama za vidole ulioboreshwa zaidi kwa ajili ya ulinzi wa taarifa binafsi za mmiliki wa simu.
Post a Comment