Mgombea nafasi hiyo mwaka 2010, Profesa Ibrahim Lipumba.
Na Mwandishi Wetu HUKU joto la
uchaguzi mkuu wa urais mwakani likiwa nyuzi mia moja tayari, uchunguzi
umeonesha mgombea nafasi hiyo mwaka 2010, Profesa Ibrahim Lipumba kwa
tiketi ya Chama cha Wananchi (Cuf) nafasi hiyo haimtaki tena.
Baadhi ya wapenda mambo ya siasa waliozungumza na gazeti hili
mwanzoni mwa wiki hii walitoa maoni yao wakisema wanaunga mkono muungano
wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa kuamua kumsimamisha mgombea
mmoja mwakani.
Hata hivyo, walisema kwa maoni yao, hata kama hayatapita, Lipumba
hafai kusimama katika nafasi hiyo na kugombea tena katika kipindi cha
kuingia mwaka wa ishirini na tano.
“Lipumba angepumzika, awaachie wengine. Aligombea mara ya kwanza
mwaka 1995 na Mkapa (Benjamini) wa Chama cha Mapinduzi. Akagombea naye
tena mwaka 2000 na Mkapa huyohuyo.
“Mwaka 2005 akagombea na Kikwete (Jakaya) wa CCM, mwaka 2010
akagombea naye tena. Kama Cuf watamsimamisha mwakani ina maana atakuwa
anagombea urais kwa mara ya tano akiwa anaenda mwaka wa ishirini na
tano, si sawasawa,” alisema mdau mmoja.
Uchunguzi zaidi unaonesha kuwa, kuna watoto walizaliwa wakati Lipumba
anaanza kugombea urais mwaka 1995 na mwakani vijana hao watakuwa na
sifa ya kupiga kura kuchagua rais. Lo!
Kumbukumbu zinaonesha kuwa, mwaka 1995, Lipumba alipata kura za urais 418, 973 sawa na asilimia 6.43. Mwaka 2000 alipata kura 1,329,077 sawa na asilimia 16.26.
Kumbukumbu zinaonesha kuwa, mwaka 1995, Lipumba alipata kura za urais 418, 973 sawa na asilimia 6.43. Mwaka 2000 alipata kura 1,329,077 sawa na asilimia 16.26.
Mwaka 2005 alipata kura 1, 327,125 sawa na asilimia 11.68 na mwaka 2010 alipata kura 695,667 ambapo ni sawa na asilimia 8.06.
Post a Comment