MISUKULE YA GWAJIMA KUFIKISHWA MAHAKAMANI! SOMA ZAIDI HAPA


Misukule ya Gwajima Yatinga Polisi.....Ndugu, Wazazi kuitwa ili kuthibitisha vifo vyao. Baada  ya  hivi  karibuni  kutoa  waraka  mzito  unaowalenga  watumishi  wa  mungu  kwa  kile  alichodai  kuwa  ni  ukiukwaji  wa  sheria  za  mungu, Nabii Hosea  Chamungu  ametangaza  rasmi  kuiwasilisha  ripoti  ya  misukule  feki  mikononi  mwa  jeshi  la  polisi  ili  hatua  za  kisheria  zichukuliwe....


Akiongea  kwa  kujiamini, Nabii  ChaMungu  alimuonyesha  mwandishi  baadhi  ya  picha  za  misukule  ikiwemo  iliyowahi  kuonyeshwa  ndani  ya  kanisa  la  ufufuo  na  uzima  linaloongozwa  na  mchungaji  Josephat  Gwajima..
"Unapofanya  kazi  ya  mungu  hutakiwi  kuwa  mwoga  kwa  lolote  kwani  yeye  ndiye  anayetulinda  sisi  sote, kondoo  wa  bwana  wamekuwa  wakipotea  siku  hadi  siku  huku  wachungaji  tukiwaangalia  bila  kuwaokoa.Mimi  sikubaliani  na  hii  miujiza  ya  kutoa  misukule  inayotangazwa  kila  siku  wakati  hatujui  hao  misukule  walifia  wapi....

"Baada  ya  kufunuliwa  na  mungu  juu  ya  jambo  hili, nimeanza  kukusanya  taarifa  kuhusiaa  na  hili  jambo  na  tayari  uelekeo umeshapatikana, watu  hawataamini  siku  nitakapoliweka  wazi  hili  suala  kwani  nitaliomba  jeshi  la  polisi  liwashitaki  wote  waliorubuniwa  na  kujifanya  misukule  pamoja  na  wale  walioinjinia  ishu  nzima.Kama  kuna  watu  wenye  uwezo  wa  kufufua  watu  kwa  nini  vifo  vinaendelea  kutokea  kila  siku?",alisema  Cha Mungu.Cha  Mungu  alidai kuwa  zoezi  hilo  litafikia  hitimisho  mwishoni  mwa  mwezi  ujao.

Aidha, alitoa  wito  kwa  ndugu, jamaa  na  wazazi  ambao  kwa  namna  moja  au  nyingine  wamehusika  na  kuficha  siri  za  ndugu, jamaa  au  watoto  wao  waliojihusisha  na  zoezi  la  kumdhihaki  Mungu  la  kujifanya  wao  ni  misukule  wangali  wakijua  si  kweli  wajisalimishe  kabla  hajawaumbua....

"Nitakapokamilisha  details  nitawataja  kwa  majina, mahali  walipo  na  jinsi  walivyohusika, kwa  wale  ambao  wanaogopa  vitisho  waje  nitawaombea  na  roho  ya  woga  itaondoka  na  hakuna  atakayewadhuru," alisema.Jitihada  za  kumpata  mchungaji  Gwajima  kuongelea  suala  hilo  ziligonga  mwamba  kutokana  na  simu  yake  kutopatikana

Post a Comment

Previous Post Next Post