KAMATI YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA YAMALIZA ZIARA YAKE KATIKA MGODI WA BUZWAGI

 Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira hii leo imekamilisha ziara yake kwa kukagua mgodi wa Buzwagi na kuridhishwa na utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na usimimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa mgodi huo.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh. Ummy Mwalimu akifafanua jambo mbele ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira. Wa kwanza kulia ni Mh. James Lembeli Mwenyekiti wa Kamati hiyo.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mh. Ummy Mwalimu (katikati) akiambatana wajumbe wa Kamati katika ziara ya kukagua bwawa la kuhifadhia maji katika mgodi wa Buzwagi.

Pichani ni ujenzi wa awamu ya pili wa Kituo cha Afya cha Mwendakulima kinachojengwa na Mgodi wa Buzwagi kwa ajili ya kuwasogezea wananchi huduma bora za afya.

Baadhi nyumba zitakazotumiwa na waganga na wauguzi wa kituo cha afya cha Mwendakulima pindi kituo hicho kitakapoanza kutumika.

Post a Comment

Previous Post Next Post