Bilionea Dangote azidi kung’ara.

Aliko 
Mtandao wa Forbes umetoa list mpya ya matajiri hamsini kutoka Afrika list ambayo inaongozwa na tajiri wa Nigeria ambae ni Mfanya biashara maarufu na Rais wa kampuni ya Dangote Aliko Dangote, aliyekuwa akishikilia nafasi ya arobaini na tatu na kupanda nafasi ishirini.
Forbes imetoa taarifa hiyo na kusema Dangote pia anashikiliana nafasi ya hamsini na saba kwa watu matajiri Afrika na mtu wa pili katika watu wenye ushawishi mkubwa.
Dangote ni mfanyabiasha mkubwa anaefanya biashara za Cement, Sukari, Unga, Vinjwaji na biashara ya mafuta, bishara ambayo kwa sasa ina thamani ya Dola Bilioni ishirini na tano pia ni mfanyabiashara mweusi anayetajwa sana kati ya matajiri ishirini na tano Duniani.
Mmiliki wa kampuni ya mawasiliano ya Globacom Chief Mike Adenuga, nae ameingia katika nafasi ya pili ya matajiri Nigeria anaemiliki Dola Bilioni nne nukta sita na kushikilia nafasi ya miatatu ishirini na tano Duniani.
GENGE LAKIRI KUUA WANAFUNZI 40 MEXICO Mkuu wa sheria nchini Mexico anasema kuwa genge moja la wahalifu limekiri kuwaua zaidi ya wanafunzi 40 ambao walitoweka wiki kadha zilizopita. Jesus Murillo alisema kuwa wanachama wa genge la madawa ya kulevya la Guerreros Unidos linasema kuwa liliwaua wanafunzi hao na kisha likachoma maiti zao. Kundi hilo lilisema kuwa lilikabidhiwa wanafunzi hao na polisi baada ya makabiliano kwenye mji wa Iguala. Mkuu huyo wa sheria anasema kuwa mabaki ya maiti hizo yamepatikana kando ya mto na uchuguzi wa DNA utafanyika nchini Austria ili kuitambua. Familia za wanafunzi hao zinasema kuwa zinaamini kuwa wanafunzi hao bado wako hai. Meya wa mji wa Iguala yuko kizuizini kufuatia kuwaamrisha polisi kuingilia kati ili kuwazuia wanafunzi hao kuandamana

Make money by Copying: http://bit.ly/copy_win

Post a Comment

Previous Post Next Post