Makumbusho ya Hayati Baba wa taifa yako mbioni kupotea kwa kusahauliwa na serikali.

Makumbusho ya Hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere yako hatarini kutoweka  kufuatia  kusahaulika na serikali kushindwa kutoa fedha za kuyahifadhi licha ya Mhasisi huyo kutoa mchango mkubwa wa kulikomboa taifa na Bara la Afrika.
Akizungumza katika makumbusho ya hayati mwalimu julius kambarage nyerere kijiji cha mwitongo  wilaya ya Butiama mkoani mara muhifadhi wa  makumbusho hayo Baraka Bwire amesema anasikitishwa na serikali kutotoa fedha za kutosha kuhudumia makumbusha ya baba wa taifa huku akisema kuwa baadhi ya kumbukumbu zinaweza kutoweka kutokana na ukosefu wa vifaa na mazingira Bora ya kutunzia kumbukumbu hizo.
 
Kwa upande wake mjumbe wa kamati kuu ya chadema Grace Kiwelu amesema ni aibu kwa serikali kushindwa kuyatunza makumbusho ya Baba wa taifa na kubaki kumtaja kwa maneno huku makamu mwenyekiti wa Bawacha Hawa Mwaifunga na naibu katibu mkuu Bawacha taifa Kunti Yusuph wameitaka serikali kutumia rasilimiali alizoziacha Baba wa taifa kuboresha makumbusho hayo ili yadumu kwa ajili ya kumbukumbu ya vizazi vijavyo.
 
Baraza la wanawake wa Chadema Bawacha limetembelea makumbusho ya hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuweka mashada ya maua kwenye kaburi lake ikiwa ni ishara ya kumuenzi na kukumbuka mchango wake wa kuimarisha umoja mshikamano na uadilifu katika taifa.
- ITV

Post a Comment

Previous Post Next Post