
Akizungumza jana katika ufunguzi wa kongamano la
matumizi ya ripoti za ukaguzi kwa vyombo vya uchunguzi na wataalamu
mbalimbali, Mero alisema kongamano hilo linalofanyika kwa mara ya kwanza
ni sehemu ya utekelezaji wa shughuli za mradi wa kuongeza mapambano
dhidi ya rushwa chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Uingereza
(DFID).
Alisema kongamano hilo la siku mbili
linalowahusisha maofisa wa DCI/PCCB 40, mahakimu 20, mawakili wa
serikali 20 pamoja na wengine linalenga kutoa elimu kwa maofisa hao ili
kupambana na walaghai, walarushwa na mafisadi.
“Tukiwa wadau katika maendeleo ya nchi yetu, tunao
wajibu mkubwa wa kusimamia uwajibikaji na utawala bora. Ni vyema sasa
tukatumia fursa hii ya mahusiano ya kisheria kuboresha utendaji kazi
wetu ili kurejesha imani ya wananchi tunaowatumikia,” alisema Mero.
Aidha, alisema mpango huo utaongeza ufanisi zaidi katika utekelezaji wa matakwa ya sheria ya ukaguzi.
“Kifungu cha 27 cha sheria ya ukaguzi wa umma ya
mwaka 2008 kama kilivyofanyiwa mabadiliko na Sheria ya Fedha no. 10 ya
mwaka 2010, kinawataka wakaguzi wanaofanya kazi kwa niaba ya Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, mara tu anapobaini kuwapo kwa
viashiria vya ulaghai, kughushi au rushwa wanapokuwa wanafanya ukaguzi
kutoa taarifa kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu juu ya suala hilo,” alisema.
Post a Comment