Picha kutoka maktaba ya Rorya Kwetu
Wagonjwa
waliolazwa na kupata matibabu katika kituo cha Afya Lukole wilayani
Ngara mkoani Kagera, juzi wamejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kupata
kipigo kutoka kwa mganga wa kituo hicho ambaye aliwataka kushiriki
zoezi la usafi katika vyumba na mazingira ya kituo hicho.
Wakizungumza
na wanahabari kituoni hapo, wagonjwa hao walidai kuwa Mganga Mkuu wa
kituo hicho, Fred Nyangosie aliwapiga wagonjwa na jamaa zao akiwataka
wafanye usafi, huku wengine wakiwa ni wagonjwa wasiojiweza.
Alisema
mganga na wafanyakazi walianza kuwaburuta waliokuwa ndani ya wodi za
wagonjwa na kuamriwa kufanya usafi, huku waliokuwa wakizubaa kutafuta
zana za kufanyia usafi huo,walikuwa wakipigwa na watu kukimbia ovyo. Aidha
kijana Samweli Gwassa alisema yeye alikamatwa na mganga huyo na
kumfungia kwenye chumba maalumu kilichojulikana kuwa ni mahabusu
alipokuwa akiegesha baiskeli yake pembeni ili akachukue kwanja.Mganga
Mkuu wa kituo hicho, Fred Nyangosie hakutaka kutoa maelezo ya chanzo
cha kuwapiga wagonjwa na jamaa zao bali alidai kuwa ili aweze kuongea
lazima awe na kibali kutoka kwa mwajiri wake.Hata hivyo, Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, Colnery Ngudungi alisemaKamati ya Afya
ya Wilaya itakaa na kujadili changamoto za kituo hicho na uamuzi
utakaotolewa atawajulisha wananchi na utoaji huduma unaendelea.
crd: mishemishe za mwafrika
Mmoja wa
wagonjwa hao, Ester Bonifasi aliyekuwa akipata matibabu katika kituo
hicho, alisema kituoni hapo kuna utaratibu wa kuzuia wagonjwa kulia
chakula wodini, hivyo walipokutwa wakikiuka utaratibu huo walianza
kupigwa na mganga huyo.
Post a Comment