Habari wadau, naomba kuwajulisha kuwa mwili
wa mwandishi wa zamani wa michezo, Innocent Munyuku aliyefariki dunia juzi, unaagwa
leo Ijumaa kuanzia saa tano asubuhi hospitali ya Jeshi Lugalo, Dar es Salaam
kabla ya kusafirishwa kwenda Morogoro kwa mazishi.
Pia mwili wa mwanachama wa Chama cha
Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Baraka Karashani, aliyefariki
juzi utazikwa kesho Jumamosi makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam badala ya leo
makaburi Sinza kama ilivyokuwa imetangazwa jana. Msiba upo nyumbani kwa wazazi
wa marehemu maeneo ya Mawasiliano Tower, barabara ya Sam Nujoma, Ubungo Dar es
Salaam.
Nawasilisha,
Katibu Mkuu TASWA
21/11/2014
Post a Comment