Innocent Munyuku kuagwa leo saa 5 Lugalo

Habari wadau, naomba kuwajulisha kuwa mwili wa mwandishi wa zamani wa michezo, Innocent Munyuku aliyefariki dunia juzi, unaagwa leo Ijumaa kuanzia saa tano asubuhi hospitali ya Jeshi Lugalo, Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kwenda Morogoro kwa mazishi.
Pia mwili wa mwanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Baraka Karashani, aliyefariki juzi utazikwa kesho Jumamosi makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam badala ya leo makaburi Sinza kama ilivyokuwa imetangazwa jana. Msiba upo nyumbani kwa wazazi wa marehemu maeneo ya Mawasiliano Tower, barabara ya Sam Nujoma, Ubungo Dar es Salaam.
Nawasilisha,
Katibu Mkuu TASWA
21/11/2014

Post a Comment

Previous Post Next Post