Machimbo ya vito Mto Muhuwesi yaua watatu

VIJANA watatu waliokuwa wanafanya kjazi ya kuchimba madini katika kiwanja kinachomilikiwa na Mchimbaji mdogo aliyefahamika kwa jina la Christofer Simkoko wamekufa baada ya kuangukiwa na kifusi cha udongo.
Taarifa zilizotolewa na Msimamizi wa machimbo hayo yaliyopo katika eneo la Mto Muhuwesi maarufu kwa jina la namba saba Bw. Hamisi Ibrahim Yasini alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 4.30 asubuhi ya Novemba 20 mwaka huu .
Bw. Yasini aliendelea kufafanua kuwa tukio hilo lilitokea wakati vijana hao wakitoa udongo wenye madini ya vito ( Veny).
Alisema baada ya kutokea kwa tukio hilo yeye kwa kushirikiana na wachimbaji wengine walijitahidi kujaribu kuokoa maisha ya wenzao kwa kuanza kuchimba na kutoa udongo huo kwa kutumia chepe na mikono hali ambayo iliwafanya washindwe kuwaokoa wakiwa wazima kutokana na kutokuwa na nyenzo zenye uwezo mkubwa kiutendaji.
Kwa mujibu wa Ibrahi wachimbaji waliopoteza maisha ni wakazi wa Wilaya ya Vijiji vya Wilaya ya Tunduru na kuwataja kuwa ni Rashid Sandali (30) mkazi wa Kijiji cha Legezamwendo,Ibrahim Husein (34) mkazi wa kijiji cha mwongozo na Kaluma Ally (35) Mkazi wa kijiji cha Namasalau wilayani humo.
Akizungumza na wachimbaji wa madini hayo alipotembelea katika eneo la tukio hilo Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Bw. Chande Bakari Nalicho pamoja na mambo mengine alisema Pamoja na Serikali kupenda watu wake kupenda wapate fedha ili kuendesha maisha yao kwa kula raha na starehe, lakini haiwezekani kuona wananchi wake wakipoteza maisha kama lilivyo tokea tukio hilo kwa kisingizio cha kutafuta fedha.
 Akizungumzia tukio hilo kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Mihayok Msikhela pamoja na kudhibitisha kuwepo kwa tukio hilo aliwataka wachimbaji katika mkoa wake kuzingatia taratibu za uchimbaji wa madini hayo pamoja na kuzingatia maelekezo na taratibu za uchimbaji salama.
Source: Steven Chindiye, Tunduru

Post a Comment

أحدث أقدم