MBOWE NA KITENDAWILI CHA MGOMBEA WA URAIS NDANI YA UKAWA


MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Freeman Mbowe, amesema bado hawana mgombea wa urais  ndani ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA),kwa vile wanaendelea kuweka  utaratibu mzuri zaidi  wa kushiriksha kwa wanachama wao ili kumpata mtu mwenye sifa na kukubalika kwa wananchi wote  katika kuwania kugombea urais wa mwaka 2015.
Hivyo amesema , wakati ukifika  mtu yotote kutoka ndani ya umoja wao bila kujali wadhifa wake watakuwa na fursa ya kujitokeza kuwania nafasi hiyo na atakayeonekana  anafaa na kukubalika kutokana na  sifa, uadilifu na uzalendo  ataombwa atangulie  mbele.
Mwenyekiti huyo wa Taifa wa Chadema alisema hayo juzi , wakati akiwahutubia mamia ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika katika  uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, Manispaa ya Morogoro ambao ukiwa ni mkutano wake  mwisho  baada ya kuzunguka mikoa mbalimbali nchini na kijiti kumkabidhi Katibu Mkuu wake kuendeleza ziara hizo.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema kuwa, ushirikiano wa vyama hivyo vinne si wa viongozi pekee badi ni vya wanachama na wananchi kwa ujumla wao ambao wanakiu ya kupata mabadiriko .
“ Kilio cha ushirikiano huu si cha Mbowe au Lipumba na viongozi wengine wa Ukawa  na hatuendi na Ukawa ili kugawana vyeo , bali ni kuweka msingi wa kumsimamisha mwenye uwezo na wengi wakimkubali...ataambiwa atangulie mbele kuwaongoza watanzania wenzake” alisema Mbowe.
 Pamoja na kusema, Ukawa haipo kwa misingi ya  kugawana vyeo, alisema upo kwa ajili ya kujenga nchi na hata walipo nje ya umoja wao na hata wanaCCM wenye kupinga ufisadi wanaweza kuingia kushiriki katika harakati za ukombozi wa Taifa.
Hata hivyo aliwataka wanachama wa Chadema kuacha tofauti ya vyama bali wote waunganishe nguvu zao kuwashawishi wanaCCM ambao wanachukizwa na matendo ya viongozi wao washiriki katika mapambano kulirejesha taifa kuwa na viongozi wanaofuata  msingi  ya kimaadili.
“ Taifa hili lina mpasuko kutokana na vyama vingi ambavyo vinawagawa wananchi kiitikadi na rangi za bendera na kusahau kujenga umoja wakutetea maslahi ya wananchi wanyonge” alisema Mbowe na kuongeza kuwa.
Naye Naibu Katibu Mkuu Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu , alisema kuwa Chadema hakikatai mfumo wa wananchi katika kuchangia shughuli za maeneleo bali kinachosisitiza ni kwamba fedha zinazopatikana zitumike kuwalekea maendeleo wananchi wake na si kutajirisha kundi la viongozi wachache.
Kwa mujibu wa Naibu Katibu Mkuu huyo wa Chadema Zanzibar,uchangiaji wa shughuli za maendeleo ulikuwepo hata katika serikali ya awamu ya kwanza na Mwalimu Julius Kambarege Nyerere, lakini matunda ya uchangiaji huo yalionekana kwa uboreshaji wa huduma za kijamii, elimu, afya na maji.
Hivyo alisema , ni wajibu wa Serikali inapokusanya kodi ,  ziwanufaishe wananchi katika kuboresha maendeleo yao badala yakuachiwa wananchi kugharamia uchangiaji wa kila jambo.
SOURCE: John Nditi, HABARILEO Morogoro

Post a Comment

Previous Post Next Post