Mchezo wa Kirafiki wa Kimataifa Veterani wa Zanzibar na wa Nigeria Amaa


Kikosi cha timu ya Zanzibar Veterani kilichotoana jasho na timu ya Nigeria Veterani katika uwanja wa Amaan Zanzibar katika mchezo wao wa kirafiki wa kimataifa kukuza mchezo huo Visiwani na kutowa hamasa kwa Wachezaji Vijana kuinua viwango vyao vya mchezo na Zanzibar kwa jumla.
Kikosi cha timu ya Nigeria Veterani waliotoa sare na timu ya Zanzibar Veterani wakionesha mchezo mzuri na wakitaalam kuonesha wakati wao jinsi mpira uliovyokuwa ukichezwa. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi na Utumishi wa Umma Mhe. Haroun Ali Suleiman, akisalimiana na wachezaji wa Zanzibar Veterani akimpa mkono mchezaji Amour Azizi (Kijeba) kabla ya kuaza kwa mchezo huo wa kimataifa uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi na Utumishi wa Umma Mhe. Haroun Ali Suleiman, akisalimiana na wachezaji wa Zanzibar Veterani akimpa mkono mchezaji Haji Mwinyi kabla ya kuaza kwa mchezo huo wa kimataifa uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar. 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi na Utumishi wa Umma Mhe. Haroun Ali Suleiman, akisalimiana na wachezaji wa Nigeria Veterani akimpa mkono mchezaji Poubeni Ogun, kabla ya kuaza kwa mchezo huo wa kimataifa uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi na Utumishi wa Umma Mhe. Haroun Ali Suleiman, akisalimiana na wachezaji wa Nigeria Veterani akiwatambulisha nahodha wa timu hiyo, Poubeni Ogun, kabla ya kuaza kwa mchezo huo wa kimataifa uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar. 
Wachezaji wa timu ya Zanzibar Veterani wakisalimiana na wachezaji wa Nigeria Veterani kabla ya kuaza kwa mchezo wao wa kirafiki wa Kimataifa uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar.
Mchezaji mkongwe wa Timu ya Taifa ya Zanzibar na Tanzania Shabani Ramadhani akisalimiana na Mshauri Ufundi wa Nigeria Veterani Engr. Iyenemi N Ameiye, kabla ya kuaza kwa mchezo huo uliofanyika uwanja wa amaan. 
          Mchezaji wa Zanzibar Veterani Waziri Seif, akimpita beki wa Nigeria Veterani Singa.
Mchezaji wa Veterani Zanzibar Haji Mwinyi akifudga balo la kwanza kwa timu yake dhidi ya timu ya Nigeria Veterani. katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika uwanja wa amaan.  

Post a Comment

Previous Post Next Post