Unanicheka, ati ninauliza swali la kitoto sana kama siyo la
kijinga, kwani kwa ufahamu wako, akili yako na hata kwa hali ya kawaida
tu; unaamini ya kuwa kila mtu anajua ya kwamba ‘kahaba’ ni mwanamke
basi!
Nasema hivyo kwani hata mimi mwenyewe niseme
nilipoanza kuchipukiwa niliamini hivyo kuwa kahaba ni mwanamke; na wala
sikusumbua akili yangu kutaka kujua ni mwanamke ki-vipi? Na kwa nini, na
nililiona kuwa jina ‘kahaba’ ni dhahiri kwa wanawake.
Wapo wanajamii wanaokwenda mbali zaidi kifikra ya
kwamba ‘makahaba’ ni baadhi ya wanawake wengi wanaoishi mjini; wengine
huamini ya kuwa wasichana ambao hawajaolewa na wanafanya kazi mjini basi
wote ni ‘makahaba’. Hii siyo kweli.
Dhana potofu
Kumekuwa na dhana potofu au kujengeka kwa uonaji
wa kimoyomoyo bila yakuwa na uhakika ya kwamba binti yeyote “anapovunja
ungo”, neno hilo hutumika kwa wasichana wanapo balehe, basi jambo
lifuatalo ama haki ifuatayo kwao ni kuolewea tu.
Dhana hiyo imejengeka mno ndani ya jamii zetu
miaka nenda-rudi hasa huko vijijini na imekuwa ikitekelezwa hivyo, pia
baadhi ya makabila bila ya kuchelea ama niseme hakuna sumile kwa hilo.
Kutokana na dhana hiyo potofu baadhi hata niseme
wasichana wengi wanapokosa kwa lugha ya kijijini “mtu wa kuwatokea”,
yaani kupeleka barua ya posa hujiona kuwa hawana bahati au ni ‘mkosi’
kwao na kujijengea upweke wa maisha. Hali hiyo huweza kabisa kuwaletea
kishawishi cha kuhamia mjini wakidhani huko wanaweza kupata bahati ya
kuolewa kwa minajili ya kutojulikana na wanaume wa mjini juu ya makuzi
yao ya awali.
Kahaba ni nani
Ni mtu wanaume au mwanamke anayeshiriki mambo ya
uasherati kuwa ni biashara au starehe yake; malaya, mtembezi, mzinifu na
mzinzi. Kwa maana hiyo basi hata wewe mwanaume unaesoma makala hii
unaweza kuwa ‘kahaba’ ingawa wengi wanaliona hilo likiwaangukiwa baadhi
ya wanaume wenye tabia au wanaofanya mambo ya ‘kike-kike’ almaarufu kama
‘mashoga’. Soma Biblia Mwanzo 19:1-29, uchafu wa miji ya Sodoma na
Gomora, ukiwahusisha wanaume wenye tabia hizo, miji hiyo ilichomwa moto
na Mwenyezi Mungu.
Kwa wanaume ‘starehe’ hiyo ya uzinifu kwa wengi
wanaiona ni sifa ya kuwa rijali na wala hawaioni kuwa ni starehe chafu
inayowaunganisha kwenye kundi hilo la ‘ukahaba’. Pia, hii nayo imejengwa
kwenye dhana potofu ya kuwa wanaume ni viumbe wa viwango vya juu dhidi
ya wanawake; na kuwachukulia wanawake kama ni ‘chombo’ cha starehe kwao,
hivyo wao wanaume hawastahili kuitwa ‘makahaba’. Ni makahaba pia.
Uonevu wa dhati
Kutokana na hali ngumu ya maisha hasa kwa
wanawake-madada, inayosababishwa na uonevu huu kuwa wao ni kiumbe cha
daraja la pili, vipaumbele kwa mambo mengi ya kijamii yamelengwa kwa
wanaume ingawa ni kimyakimya; sasa Serikali inapiga baragumu la usawa
usiotimilizwa sawasawa.
- Mwananchi
- Mwananchi
Post a Comment