Jumuia ya waTanzania Washington, D. C., Maryland na Virginia (DMV) imefungiwa na D. C. Department of Consumer and Regulatory Affairs (DCRA).
Hadi hivi sasa haijulikani ni sababu gani iliyo pelekea kufungiwa kwa
jumuhiya hii. Wakiongea kwenye mtandao wa Viber baadhi ya wakazi wa DMV
walijaribu kumuuliza maswali Ndg. Idd Sandaly juu ya ni kwanini Jumuia
imefungiwa;Ndg. Sandaly alishindwa kutoa majibu. Hadi hivi sasa si Ndg.
Sandaly wala Bodi ya wadhamini aliye toa ufafanuzi juu ya kwa nini
jumuhiya imefungiwa. Chini ni makaratasi kutoka DCRA yanayo onyesha
kufungiwa kwa jumuhiya ya waTanzania DMV
Post a Comment