Na Imelda Mtema MSANII
 anayekuja kwa kasi katika tasnia ya Filamu Bongo, Sarbrina Omary ‘Sabby
 Angel’ amefunguka kuwa  mwanamuziki, Rummy Nanji ‘Bob Junior’ ambaye 
kwa hivi sasa ndiye mpenzi wake amembadilisha mavazi yake aliyokuwa 
akivaa awali kabla hawajawa pamoja.


Msanii anayekuja kwa kasi katika tasnia ya Filamu Bongo, Sarbrina Omary ‘Sabby Angel’ akipozi.
Akizungumza na Amani, Sabby alisema kuwa mpenzi wake huyo mara nyingi
 anapenda ajitande nguo na kuwa mtoto wa Kiislamu kama asipokuwa katika 
ishu za kurekodi kwani anaamini kuwa binti wa Kiislamu anapaswa kuvaa 
kiheshima.
Mtoto ‘Sabby Angel’ akiwa na Nanji ‘Bob Junior’.
“Nimekamatika sana, yale mavazi yangu ya awali nimeambiwa ‘stop,’ 
tukiwa katika mazingira ya kawaida ni lazima nijitande na nionekana 
haswa ni mtoto wa Kiislamu,” alisema  Sabby.
Post a Comment