Ustadh Khalid Mwarangi, Imam wa Masjid Bilal ulioko mtaa wa Maranza, wilaya ya
Likoni,nchini Kenya ameuawa kwa kupigwa risasi na watu waliokuwa katika
pikipiki usiku huu.
Katibu
wa mtaa wa Maranza, Kassim Mwamgula amethibitisha kutokea kwa tukio
hilo na kuongeza kueleza kuwa Ustadh Mwarangi amekufa alipokuwa
wanampeleka katika hospitali ya wilaya ya Likoni.
Mwamgula
ameeleza kuwa watu wawili waliokuwa katika pikipiki walimlenga risasi
marehemu alipokuwa akielekea msikitini wakati wa swala ya Isha.
"Mwanzo
kulipita landcruiser ya polisi baadaye kidogo watu waliokuwa na
pikipiki walifika wakageuza pikipiki wakampiga risasi" amesema Mwamgula.
Post a Comment