
Wananchi hao walioonekana kukerwa na jinsi mjadala
mzima ulivyovurugika kutokana na kiti kuyumba, walisema kwamba rasimu
ilikuwa inabainisha Spika na mawazili wasiwe wabunge ili kutenga misingi
ya uwajibikaji.
Katibu wa CUF Wilaya ya Serengeti, Vedastus
Makaranga alisema wananchi wanatakiwa kufuatilia mjadala kama huo ili
kupima uzalendo wa wawakilishi wao, kwa kuwa matatizo mengi yanachangiwa
na mfumo wa kutokuwajibika kwa viongozi wenye dhamana kwa misingi ya
kulindana kivyama.Katika hatua nyingine, wananchi hao waliwataka wabunge
wabunge kutoa uamuzi unaolenga kuleta heshima ya nchi, kwa waliohusika
na upotevu wa mabilioni ya fedha kwenye sakata la escrow.
Sospeter Mabirika Mkazi wa mjini Mugumu alisema
wabunge waache ushabiki wa vyama, kwenye suala ambalo madhara yake
yameshaanza kuonekana kwa jamii, kutokana na nchi wahisani kusitisha
uchangiaji wa bajeti ya maendeleo.
“Kila mbunge kabla ya uamuzi aangalie wapigakura
kura wake wanavyokosa huduma mbalimbali na kama fedha zilizochotwa
zingepatikana zingeweza kusaidia kutoa huduma, watu wanakimbia miji kwa
kushindwa kuchangia maabara, huku wanaohujumu wanakingiwa kifua,”
alisema.
“Haya yote yanahitaji busara ya hali ya juu katika
kuyafanyia uamuzi kwani wananchi wamekuwa wakiishi maisha magumu na
baadhi yao wakifaidika na rasilimali za nchi.’’
إرسال تعليق